Posts

Showing posts from January, 2025

ULYANKULU WAPONGEZA KASI YA RAIS SAMIA KUBORESHA ELIMU

Image
         Na Allan Kitwe,DmNewsonline                        KALIUA  WAKAZI wa Tarafa ya Ulyankulu, Jimbo la Ulyankulu, Wilayani Kaliua Mkoani Tabora wamepongeza juhudi kubwa zinazoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya 6 kwa kuboresha miundombinu ya elimu katika vijiji na kata zote.   Wakizungumza na mwandishi wa gazeti hili kwa nyakati tofauti wameeleza kuwa Tarafa hiyo ni miongoni mwa tarafa zilizokuwa na shule chache na miundombinu hafifu lakini kasi ya serikali ya awamu ya 6 imeleta neema kubwa Jimboni humo. Mkazi wa Kata ya Ichemba Annaemmy Mazigo ambaye pia ni Mkuu wa shule ya sekondari Mkindo amempongeza Rais wa awamu ya 6 Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuipa sekta ya elimu kipaumbele kikubwa na kutenga bajeti ya kutosha. Ameeleza kuwa katika shule ya Mkindo sekondari amepeleka zaidi ya sh mil 500 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 4 na matundu 10 ya vyoo ili kuboresha miundombinu ya sh...

WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.

Image
Na Mwandishi wetu.DmNewsonline                     MARA MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Chama na serikali yake haitakubaliana na azimio lolote litakalotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kukutana kwa faragha kama walivyotangaza viongozi wa chama hicho, juzi. Amesema amesikia chama hicho kikitangaza kwamba kinakwenda kujifungia kisha kije na jambo ambalo halijapata kushuhudiwa nchini, hivyo ametoa angalizo jambo hilo ni lazima lifuate sharia za nchi. Wasira amesema hayo leo alipohutubia wananchi katika mkutano uliotumika kuzindua sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Stendi ya Zamani mjini Bunda. “Wamesema wanajifungia halafu waje wafanye jambo ambalo halijapata kuonekana, nikasema ni jambo gani, mimi nikaona huko kujifungia ile ni honeymoon maana honeymoon simnaijua, watu wakishaoana w...

RC CHALAMILA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA TRC KUONA NAMNA YA KUJENGA RELI NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline           DAR ES SALAAM  MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amesema kwamba uongozi wa  mkoa utakutana na uongozi wa  Shirika la Reli Tanzania (TRC) ili kufanya mazungumzo ya kuangalia  uwezekano wa kujenga reli yakusafirisha abiria ndani ya mkoa ili kupunguza adha ya usafiri kwa wakazi wa Jiji hilo  na  kurahisisha ufanyaji wa biashara kwa saa 24.  Hayo yamebainishwa leo Januari 30,2025 wakati wa kutoa mrejesho wa mkutano wa Nishati Afrika uliofanyika  kwa siku mbili Januari 27 na 28,2025 hapa Nchini ambapo  lengo la mazungumzo na shirika la reli ni kuangalia namna ya  kujenga reli  kwa fedha  za ndani zinazokusanywa na Halmashauri ili kupunguza adha ya usafiri. Aidha,amesema ujenzi wa reli hiyo na njia ambayo itajengwa utajulikana baada ya watalaam kufanya upembuzi yakinifu na kuona sehemu gani inapaswa kujengwa.hivyo Wataalumu watakuja na majibu. Mbali na hil...

𝗖𝗣𝗔 𝗠𝗔𝗞𝗔𝗟𝗟𝗔 𝗔𝗭𝗨𝗥𝗨 𝗞𝗔𝗕𝗨𝗥𝗜 𝗟𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘𝗠𝗨 𝗦𝗛𝗘𝗜𝗞𝗛 𝗜𝗗𝗥𝗜𝗦 𝗔𝗕𝗗𝗨𝗟 𝗪𝗔𝗞𝗜𝗟

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                 ZANZIBAR  KATIBU wa NEC Itikadi ,Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa ndugu Amos Makalla leo tarehe 30 Januari 2025 akiwa katika Muendelezo wa ziara yake Mikoa 6 ya Zanzibar ametembelea kaburi la Sheikh Idris Abdul Wakil aliyekuwa Rais wa awamu ya Nne katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar 1985 - 1990 kwenye Makaburi ya familia Kusini Unguja

RC CHALAMILA :DAR ES SALAAM KUANZA BIASHARA MASAA 24 IFIKAPO FEBRUARI 22,MWAKA HUU.

Image
Na Angelina Mganga ,DmNewsonline                    DAR ES SALAAM MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amesema wageni wote waliokuja katika mkutano wa Nishati ambao uliofanyika kwa siku mbili Jijini Dar es Salaam imeisha salama na wageni wote wameondoka salama. Amesema mikutano kama hii imezoeleka kufanyika katika nchi zingine duniani lakini kwa awamu hii Tanzania imeandaa mkutano huo kutoka katika mataifa mbalimbali ya Afrika. RC Chalamila ameyasema hayo leo Januari 30 ,2025 mbele ya waandishi wa habari  Jijini Dar es Salaam amesema mkutano huo umeleta tija kubwa kwa Mkoa wetu kwa Yale yote  ambayo yamefanikiwa ni wazi kwamba Kuna mafanikio makubwa hususani.katika eneo la miundombinu ya umeme  Pia amesema Jiji la Dar es salaam litaanza kufanya shughuli za biashara kwa masaa 24 ambapo uzinduzi utafanyika Februari 22,2025 wafanyabiashara  wataanza rasmi. Aidha ,amesema  zoezi hilo limechelewakuwa kwasaba...

TAKUKURU TABORA WABAINI MADUDU KWENYE MIRADI YA MAENDELEO

Image
        Na Allan KitweDmNewsonline                             TABORA  TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Tabora imetembelea na kukagua jumla ya miradi 11 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya sh bil 28 na kubaini dosari katika utekelezaji baadhi ya miradi hiyo. Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoani hapa Abnery Mganga amesema kuwa taasisi hiyo imebaini mapungufu katika miradi 8 kati ya 11 iliyochunguzwa kutokana na dosari mbalimbali za kiutekelezaji. Ameeleza kuwa miradi hiyo yenye thamani ya zaidi ya sh bil 27 iliyotekelezwa katika Wilaya zote za Mkoa huo ni ya ujenzi wa shule (vyumba vya madarasa) katika shule za msingi na sekondari kupitia mradi wa SEQUIP na BOOST. ‘Naipongeza serikali kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za utekelezaji miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali, ni jukumu la taasisi hii kuhakikisha fedha zote zinazol...

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTOKOMEZA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline          DAR ES SALAAM  SERIKALI kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa mwaka 2024 wameweza kutoa dawa za kingatiba za kudhibiti na kutokomeza magonjwa mbalimbali. Magonjwa hayo  kama Watu 257,358 kati ya 265,217 walipatiwa kingatiba za kutokomeza ugonjwa wa matende na mabusha kutoka kwenye Halmashauri za Mtama na Mtwara Mikindani (sawa na asilimia 97),. Watu 5,462,851 kati ya 6,447,157 kutoka katika Halmashauri ishirini na nne (24) walipatiwa kingatiba ya ugonjwa wa Usubi (sawa na asilimia 85), watu 1,603,425 kati ya 1,967,143 kutoka Halmashauri saba (7) Halmashauri hizo ni Ngorongoro DC Monduli DC, Longido DC, Kiteto DC, Simanjiro DC, Mpwapwa DC na Kalambo DC, walipatiwa kingatiba za ugonjwa wa trakoma sawa na asilimia 82. Watoto wenye umri wa kwenda shule (yaani umri wa miaka 5-14) 9,896.694 walilengwa kupatiwa huduma ya kingatiba kwa ugonjwa wa minyoo ya tumbo ambapo hadi kufikia Disemba 2024 watoto 8,676,234 sawa n...

DKT. BITEKO AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MIILI YA WANAFUNZI WALIOFARIKI KWA RADI GEITA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                   GEITA LEO  Januari 30, 2025 mkoani Geita, maelfu ya waombolezaji wamejitokeza kuaga miili ya wanafunzi saba wa Shule ya Sekondari Businda iliyopo wilayani Bukombe waliofariki kwa kupigwa na radi mnamo tarehe 27 januari, 2025.  Rais Samia atuma salamu za pole,  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameongoza shughuli za kuaga na kukabidhi ubani kwa wafiwa huku akiwataka kuwa wavumilivu hasa kipindi hiki cha majonzi. Ametoa pole kwa wazazi, walezi ndugu wa watoto pamoja na wanafunzi wa Businda kwa kuondokewa na wapendwa wao na wanajamii wa Businda Sekondari kwa jitihada na utoaji wa huduma wakati wa tukio hilo. “ Imeandikwa kwamba shukuruni Mungu kwa kila jambo, Mungu ametukutanisha leo katika hali ya majonzi. Tukio hili litukumbushe kutenda mema wakati wote na tuamini kwamba Mungu ndiye mwenye uweza. Kipekee ningetam...

ASKOFU AMANI ACHUKIZWA NA UTORO WANAFUNZI VYUONI, ATOA WITO KWA WAZAZI

Image
Azindua Gereji ya St.Gabriel, chuo cha ushonaji na ufundi wa magari    - Atoa wito kwa wakazi wa Arusha kupeleka magari mabovu    Na Seif Mangwangi,DmNwwsonline                ARUSHA ASKOFU wa jimbo kuu Katoliki Arusha, Mhashamu Askofu Issack Amani amedai kuchukizwa na utoro wa vijana wanaopata nafasi ya kusomeshwa katika vyuo mbalimbali nchini ili kupata ujuzi na kuweza kuajiriwa na hivyo kutoa wito kwa wazazi kuwa karibu na vijana wao kuwafunza maadili. Pia amewataka vijana wanaopata nafasi ya kusoma hususani ngazi ya ufundi katika vyuo tofauti nchini kuzingatia masomo yao kwa kuwa Wasomi ni wengi mtaani na ajira zimekua ngumu kupatikana. Akizungumza jijini humo Januari 29, 2025 wakati wa uzinduzi wa chuo cha ushonaji na chuo cha ufundi wa magari cha Mtakatifu Gabriel kinachoendeshwa chini ya kanisa Katoliki parokia ya Moyo Safi Unga Limited, Askofu Amani amesema wanafunzi wanapaswa kuwa wabunifu ili waweze kupata ajira. Asko...

WAZIRI WA ELIMU PROF.MKENDA:SERA YA ELIMU SASA KUZINDULIWA FEBRUARI 1,2025.

Image
Na Deborah Lemmubi.DmNewsonline                 DODOMA  WAZIRI wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof.Adolph Mkenda mapema Leo hii ametangaza mabadiliko madogo kwenye tukio la Uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023 uliotakiwa kufanyika kesho tarehe 31 Januari 2025 na utafanyika tarehe 1 Februari 2025 kutokana na dharula ambayo imeshindwa kuzuilika na kufanya ratiba hiyo kusogezwa kidogo. Waziri ameyasema leo Januari 30,2025 alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mabadiliko yaliyojitokeza katika kuelekea Uzinduzi huo. Na kuongeza kuwa pamoja mabadiliko hayo ya tarehe mpya 1 Februari lakini Mgeni rasmi bado atabaki kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan.  "Leo nimewaita hapa kueleza mabadiliko kidogo kwenye tukio la Uzinduzi wa Sera ya Elimu ambalo lilikuwa lifanyike kesho Januari 31 2025,lakini kwasababu ya dharula  ambayo imeshindwa kuzuilika tukio hilo sasa lonas...