SERIKALI YATOA BILIONI 24 KUBORESHA UWANJA WA NDEGE TABORA
![Image](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiU5ImAnj74WYfNUrVrruEr01BbYkqQKUtRIJp_xK8LKA74zgV0QCqWsJnOJ2zRiy2-cm95wjnGmiBtYIANvslYvpy-RkFBlV8wK9x9GbFdfHucXFHCyU9rhg_bofPyAKan_YH5S9tbbRg/s1600/IMG_ORG_1706722863661.jpeg)
Na Allan Vicent,DmNewsOnline TABORA SERIKALI ya awamu ya 6 inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa kiasi cha sh bil 24.6 kwa ajili ya ukarabati na uboreshaji uwanja wa ndege Tabora ambapo jengo jipya la abiria la ghorofa mbili limeanza kujengwa. Akizungumza baada ya kutembelea uwanja huo juzi, Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amemshukuru Rais Samia kwa kuwapatia kiasi hicho cha fedha ili kuufanyia maboresho makubwa uwanja huo. Amebainisha kuwa mradi huo ambao umeanza kutekelezwa mwaka jana unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu hivyo kuwezesha ndege nyingi na kubwa kutua katika uwanja huo na kupatikana huduma muhimu zote. ‘Mkandarasi alitakiwa kumaliza kazi hii mwezi Machi 2024 lakini ameomba kuongezewa muda zaidi kutokana na vifaa vilivyoagizwa kutoka nchini India na China kuchelewa kufika’, alisema. Profesa Mbarawa amemwagiza Mkandarasi anayetekeleza mradi huo Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group Company Ltd kuhakikisha ...