Posts

Showing posts from December, 2024

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA ASHIRIKI DUA YA KUMUOMBEA MAREHEMU MHE. JAJI MWANAISHA KWARIKO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga ameshiriki dua maalum ya kumuombea marehemu Mheshimiwa Mwanaisha Athumani Kwariko, Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (INEC) Tarehe 29 Disemba, 2024 nyumbani kwake Masaki Jijini Dar es Salaam. Dua hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo, Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Profesa Ibrahim Juma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. James Henry Kilabuko, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mhe. Jaji George Kazi pamoja na baadhi ya wajumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania akiwemo, Mhe. Asina Omari na Mhe. Balozi Omary Mapuri. Akitoa salamu wakati wa dua hiyo Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Profesa Ibrahim Juma ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote waliofikwa na msiba huo hu...

WATAALAMU WA LISHE IGUNGA WATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU

Image
Na Allan Kitwe,DmNewsOnline TABORA  WATAALAMU wa Lishe katika halmashauri ya Wilaya ya Igunga Mkoani hapa wametakiwa kuongeza ubunifu utakaoleta matokeo chanya miongoni mwa jamii ikiwemo kuboreshwa afya zao. Rai hiyo imetolewa juzi na Mkuu wa Wilaya hiyo Sauda Mtondoo alipokuwa akifungua Kikao cha Wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilayani humo ambacho pia kilikuwa na jukumu na kujadili bajeti ya kufanikisha majukumu yao. Sauda amesisitiza kuwa Kamati hiyo ni muhimu sana kwa kuwa imebeba maslahi ya afya za wakazi wa Wilaya hiyo, hivyo akaelekeza Wajumbe wa Kamati hiyo kuja na mikakati chanya na inayotekelezeka kwa manufaa ya wananchi. Amebainisha kuwa moja ya mikakati ya halmashauri hiyo ni kuongeza uzalishaji wa chakula lishe ili kujenga afya za wananchi na kupunguza tatizo la utapiamlo na magonjwa yanayotokana na ukosefu wa lishe. ‘Kikao hiki ni muhimu sana kwa kuwa kinajadili maslahi mapana ya jamii na afya zao, naamini bajeti itakayopitishwa itazingatia malengo ya halmashauri ya kuima...

ANJITA YAVIWEZESHA VIKUNDI VYA KILIMO CHA BUSTANI ZA MBOGAMBOGA PEMBEJEO ZA MILIONI SHILINGI MILIONI 10.7

Image
Na Mwandishi Wetu, DmNewsOnline. PWANI  TAASISI ya Anjita Child Development Foundation ya Kibaha imetoa pembejeo za milioni 10.7 kwa wakulima wa bustani za mbogamboga. Wakulima hao wa bustani ni vikundi ambavyo vinatoka kwenye Vitongoji vya Mwanabwito na Kidai Kata ya Kikongo Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani.  Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi kuwezesha jamii kupitia kilimo cha bustani na kukabidhi pembejeo  kwa vikundi hivyo Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Evelyn Ngwira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha amevitaka vikundi hivyo kuzingatia ratiba za kilimo. Ngwira amesema kuwa mradi huo wa uwezeshaji jamii ili kujikwamua kiuchumi na kuboresha afya na utasimamiwa na wanajamii wenyewe na watapaswa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Anjita Janeth Malela amesema kuwa mradi huo umeibuliwa na wananchi wenyewe na wataundesha kwa kusimamiwa na taasisi na wataalamu wa kilimo. Malela amesema kuwa pembejeo hizo ni ufa...

SERA YA MADINI NGUZO MUHIMU KUIMARISHA SEKTA YA MADINI – MBIBO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline  MOROGORO  SERA ya Madini ya 2009 imekuwa nguzo muhimu katika kuimarisha Sekta ya Madini, japokuwa kuna haja ya kuhuisha sera hiyo ili kuendana na mabadiliko ya sasa pamoja na matarajio ya baadaye katika maendeleo ya Sekta ya Madini na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla. Hayo yamebainishwa  leo, Desemba 30, 2024 na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo wakati akiongoza Kikao cha Mapitio ya Sera ya Madini ya mwaka 2009, kilichofanyika katika Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Morogoro na kuhudhuriwa Wataalam wa Sera, na Wawakilishi wa taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa lengo la kufanya mapitio ya Sera hiyo na kuandaa mapendekezo ya maboresho. Naibu karibu  katika mazungumzo yake Amesema kuwa mchakato mapitio ya Sera ya Madini ya mwaka 2009 katika kuhakikisha Sekta ya Madini inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi nchini.  “Lengo letu ni kuhakikisha tunakuwa na Sera ya Madini inayoendana na viw...

MLAWA AWASHIKA MKONO JUMUIYA YA WAZAZI IRINGA MJINI.

Image
Eliasa Ally,DmNewsOline  IRINGA  MDAU wa Maendeleo kutoka Wilaya ya Kilolo Aidan Mlawa amechangia mifuko 50 ya saruji na mashine maalumu ya kuchapisha karatasi 'photocopy machine' kwa Jumuiya ya wazazi Iringa Mjini. Mlawa ametoa Mchango huo katika balaza la kikanuni la kufunga Mwaka alipohudhuria kama Mgeni Rasmi. "Nimesikia risala yenu kuwa mnauhitaji wa nyumba ya watumishi naomba nianze kwa kuchangia mifuko 50 ya sumenti ya kuanzia panapokwama tutaendelea kuwasiliana" Amesema  Mbali na hilo Mlawa ameahidi kuchangia mashine maalumu ya kuchapisha karatasi kwa ajili ya matumizi ya JUMUIYA. Akitoa shukrani Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Masanyika amempongeza mdau huyu kwa moyo wake wa kuchangia chama na shughuri mbalimbali za Maendeleo. "Naomba nitoe shukrani kwa niaba wa wajumbe wenzangu mchango huu ni Mkubwa sana kwetu kwa makadilio tu ni zaidi ya milioni 2 haya ni mapenzi ya dhati sana tukuahidi tu tuko pamoja na tutaendelea kushirikiana" Alisema Masanyika

WAUMINI WAASWA KUMTEGEMEA MUNGU

Image
Na Angelina Mganga ,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  KASISI wa Mtaa wa Mtakatifu Marko Malamba Mawili Mbezi Dayosisi ya Dar es Salaam Kanisa Anglikana Tanzania Rev.Fr.Kelvin Dismas amewaasa waumini wa Dini ya Kikristo kumtegemea Mungu kwani kuiona Christmas ya mwaka huu ni kwa neema ya Mungu mwenyewe. Akihubiri katika ibada ya adhimisho la kuzaliwa Yesu Kristo, Padre Dismas amesema kuzaliwa kwake  kuna makusudi mengi ikiwemo kuukomboa Ulimwengu, tena yeye ndiye asili ya  baraka,tumaini na furaha hivyo Yesu Kristo azaliwe ndani ya mioyo yetu ili makusudi ya kuja kwakwe ulimwenguni yatimie kwenye maisha yetu. "Amezaliwa kwa ajili yetu mwokozi wa ulimwengu,Yesu Kristo alizaliwa ili kuwakomboa wanadamu katika dhambi ,yeye ni mshauri wa ajabu",amesema Kasisi Dismas Aidha,amewataka waumini kutazama   kuzaliwa kwa Yesu Kristo katika namna ya rohoni zaidi.  Kristo azaliwe ndani yetu lakini kuwa na kiasi kwa mambo ya mwilini kwani pasipo na kiasi kunaweza kuleta madhara ...

CHALAMILA AWATAKIA WATANZANIA SIKUKUU NJEMA SHEREHEKEENI KWA AMANI NA UTULIVU.

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila leo Disemba 23,2024 amezungumza na waandishi wa habari na kutoa taarifa muhimu kuhusiana na maendeleo ya mkoa huo kuelekea katika sikukuu ya Christmas na Mwaka Mpya. Chalamila amewatakia  wakazi wa Dar es Salaam heri ya Christmas na mwaka Mpya na Watanzania wote kwa ujumla washerehekee kwa amani na utulivu. "Ameipongeza sekta ya habari kwa kazi kubwa na nzuri yakuipigania serikali na kuelimisha umma huku akiwatakia Wakristo na wasio wakristo kusherehekea sikukuu ya Noel kwa amani na kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani", amesema Aidha amesema kwamba vyombo vya ulinzi vimejipanga vizuri kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama katika maeneo yote ya Jiji. Pia ametoa ufafanuzi wa matukio matatu yaliyoleta taharuki katika Mkoa wa Dar es Salaam na kupelekea maswali mengi ya sintofahamu ambapo ameyataja matukio hayo ambapo tukio la mtoto aliyepotea,Jeshi la polisi lilifanya kazi kubwa ya kum...

DISEMBA 31 TAASISI ZA SERIKALI IWE MWISHO MATUMIZI YA MKAA NA KUNI.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM TAASISI zote za Serikali zilizopo katika mkoa wa Dar es salaam ambazo  zinahudumia  watu  zaidi ya 100 zimetakiwa kutekeleza bila shuruti  agizo la Waziri Kassimu Majaliwa Majaliwa  kuwa ifikapo Disemba 31,2024, ziache kutumia Nishati chafu zitokanazo  na ukataji wa kuni na mkaa .  Akizungumza leo jijini Dar es salaam,kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Albeth Chalamila ,Mstahiki Meya  wa halmashauri ya  manispaa ya Temeke Abdalah Mtinika  wakati  kuadhimisha  kilele cha wiki yakuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia ijulikayo kama rafiki briquettes inayozalishwa  na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO). Mtinika amesema kuwa kutokana na agizo hilo la Waziri Mkuu ni matumaini yake viongozi wenzake wa mkoa wa Dar es salaam watatekeleza agizo hilo bila shuruti hivyo watafanya ukaguzi kwa kila taasisi ili kuona utekelezaji wa agizo hilo. " haya tunayoyaona l...

ADEM YAUNGURUMA YATOA MISAADA KWA KAYA 13 NA WAFUNGWA BAGAMOYO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline  BAGAMOYO  KATIKA  kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita katika kuisaidia jamii   Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu-ADEM imeamua  kufanya ziara maalumu yenye lengo la  kutembelea wafungwa katika gereza la Kigongoni lilipo Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani na kutoa  misaada ya mahitaji ya msingi na vitu mbalimbali ambavyo vitawasaidia katika gereza hilo.  Akizunngumza Katika ziara hiyo mkurugenzi wa taaluma wa ADEM Bugendi Joseph amesema  kwamba  wamepata  fursa ya kutembelea gereza hilo na kutoa mahitaji kama vile  miswaki, dawa za meno, viwembe, sabuni, unga na mchele  kwa kuzingatia mahitaji ya wafungwa. Pia Bugendi amebainisha kwamba mbali na kutembelea gereza hilo pia  watumishi pamoja na wanafunzi wa ADEM wametembelea kituo cha kulelea watoto wanaotoka katika mazingira magumu cha  Amani Orphanage Center kilichopo katika Kata ya Zinga Wilayani Bagamoyo na ku...