DISEMBA 31 TAASISI ZA SERIKALI IWE MWISHO MATUMIZI YA MKAA NA KUNI.



Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM

TAASISI zote za Serikali zilizopo katika mkoa wa Dar es salaam ambazo  zinahudumia  watu  zaidi ya 100 zimetakiwa kutekeleza bila shuruti  agizo la Waziri Kassimu Majaliwa Majaliwa  kuwa ifikapo Disemba 31,2024, ziache kutumia Nishati chafu zitokanazo  na ukataji wa kuni na mkaa . 

Akizungumza leo jijini Dar es salaam,kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Albeth Chalamila ,Mstahiki Meya  wa halmashauri ya  manispaa ya Temeke Abdalah Mtinika  wakati  kuadhimisha  kilele cha wiki yakuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia ijulikayo kama rafiki briquettes inayozalishwa  na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).

Mtinika amesema kuwa kutokana na agizo hilo la Waziri Mkuu ni matumaini yake viongozi wenzake wa mkoa wa Dar es salaam watatekeleza agizo hilo bila shuruti hivyo watafanya ukaguzi kwa kila taasisi ili kuona utekelezaji wa agizo hilo.

" haya tunayoyaona leo ni mapinduzi makubwa katika nishati ambayo yanaenda kuacha alama kubwa kwa vizazi vyetu chini ya mbeba maono Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dkt Samia Suluhu Hassan kuhusu agenda  ya matumizi ya nishati safi na salama ili kuokoa mazingira ambapo  amekuwa ni mpambanaji wa kweli kuhakikisha jamii ya watanzania inaondokana na  matumizi ya nishati chafu ya kuni na mkaa inayotokana  na miti ifikapo mwaka 2033"Amesema Mtinika

Amesema kuwa ubora wa nishati hiyo ya rafiki briquettes  umethibitishwa na shirika la viwango Tanzania (TBS),na kufanyiwa utafiti wakutosha tangu mwaka 2018 na taasisi mbalimbali ikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es salaam,Taasisi ya Utafiti na  Maendeleo (TIRDO) pamoja na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) hivyo niwahimize wananchi kutumia nishati hii ya rafiki briquettes kutokana haina madhara yeyote kiafya.

Aidha amesema kuwa nishati hiyo ya rafiki briquettes inatokana na makaa ya mawe na kuchanganywa na vumbi la sukari guru.

"Makaa ya mawe yanazalishwa kutoka kwenye mgodi wa Kiwira unaomilikiwa na STAMICO uliopo mkoa wa Songwe ambao una hifadhi ya zaidi ya tani milioni 300 ambazo zitadumu  kwa zaidi ya miaka 100 ijayo hivyo niwatoe hofu wananchi kuwa  kuna siku  moja kutatokea uhaba wa nishati hii ya rafiki briquettes"Amesema Mtinika

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa STAMICO Dkt Venance Mwasse amesema kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi imekuwa ni tishio dunia mzima hali ambayo imepelekaifa makubwa kuweka maazimio mbalimbali ikiwemo azimio lakutunza mazingira  lakini pia azimio lakuachana na nishati chafu ambayo inaadhili afya za binadamu.

"Kupelekea maadhimio hayo mheshimiwa Rais wetu Dkt samia Suluhu Hassan alitangazwa kama kinara wakuhamasisha matumizi ya nishati safi Afrika na duniani ,sasa sisi kama stamico tulitumia ubunifu tukafanya utafiti wa bidhaa tulizonazo  ikiwemo madini tuliyo nayo,rasili mali tulizo nazo ni namna gani na tutumie teknolojia gani sayansi gani ili kubadilisha kwenda kwenye nishati safi  yakupikia ambayo hii tuliyoizindua"amesema Mwasse





Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025