Posts

Showing posts from October, 2024

TMA YATOA TAHADHARI MWENDELEZO WA MVUA ZA VULI NOVEMBA 2024 HADI APRILI ,2024

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza muelekeo wa msimu wa mvua za vuli ambazo zimeanza Novemba 2024 na kuishia mwezi Aprili,2025. Akizungumza na Waandishi wa habari  Oktoba 31 ,2024,Jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka  Dkt.Ladislaus Chang'a amesema kutokana na mabadiliko ya hali ya mifumo ya hali ya mvua nchini inaonekana kupungua kupelekea mvua katika maneno mengi kuwa chini ya wastani. Taarifa ya tahadhari imetolewa  kutokana na  mabadiliko ya hali ya hewa na mifumo mingi inaonyesha joto  kuongezeka Duniani  ukilinganisha na mwaka 2023, kwenye usawa wa Bahari maeneo mengi ya Kusini mwa Bahari ya Hindi. Msimu wa Vuli kwa miezi ya Oktoba hadi Disemba, 2024 katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka  kwa Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, Pwani ikijumuis...

AIDAN MLAWA AMPONGEZA RAIS DKT. SAMIA KWA UTENDAJI ULIOTUKUKA

Image
Na Eliasa Ally,DmNewsOline     IRINGA  MDAU wa Maendeleo wilaya ya kilolo na Mkurugenzi wa kampuni ya john Galt Hauliers LTD Usafirishaji Mizigo Ndani Nje ya Tanzania.  Aidan Mlawa ampongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kazi kubwa anayoifanya katika Taifa letu la Tanzania  Mlawa ameyasema hayo mapema wiki hii katika mahojiano na DmNewsonline ambapo amesema Rais Dkt.Samia amefanya Maendeleo makubwa ndani ya uongozi wake amepeleka Maji vijijini, umeme standad gej, Elimu bure, tren imerahisisha wafanyabiashara wanaenda Dodoma kwenda kufanyabiashara kwenda na kurudi na huduma hiyo imewarahisishia wananchi wote  Mama Samia amefanya mamiradi makubwa ndani ya nchi hii Ambapo sisi wafanyabiasha tukienda nchi za nje tukisema tunatoka nchinij Tanzania wanatamani kuja Kuwekeza Tanzania viwanda,mashamba na vitu mbalimbali  Mlawa amesema ili Mama Samia aendelee kufanya Mambo makubwa inatakiwa sisi wafanyabiashara na Wananchi inatupasa tulipe Kodi ili Rais tumu...

MIKAKATI YA RAIS SAMIA, TANZANIA KUWA NAMBA MOJA UZALISHAJI WA CHAKULA AFRIKA.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline MAREKANI Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelezea dira yake ya kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji mkubwa wa chakula barani Afrika kupitia mikakati mitatu mikuu ya Serikali katika sekta ya kilimo.  Akiwa nchini Marekani tarehe 30 Oktoba, 2024, aliposhiriki kwenye mjadala kuhusu kilimo barani Afrika katika mji wa Des Moines, Iowa, Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali yake imejizatiti kukuza sekta ya kilimo ili kufikia lengo hilo. Katika maelezo yake, Rais Dkt. Samia amebainisha mikakati mitatu muhimu ya kuendeleza kilimo kama ifuatavyo: 1. Uwekezaji katika Miundombinu ya Umwagiliaji: Serikali imepanga kuwekeza katika miradi mikubwa ya umwagiliaji ili kuhakikisha ardhi nyingi zaidi inakuwa na uwezo wa kuzalisha mazao kwa mwaka mzima. Hii inalenga kuongeza uzalishaji wa chakula na kupunguza utegemezi wa mvua. 2. Kuboresha Upatikanaji wa Teknolojia na Pembejeo za Kisasa: Ili kuongeza tija na ubora wa mazao, Serikali inashirikiana na wadau wa maendeleo kutoa ...

NAIBU KATIBU MKUU UCHUKUZI ATEMBELEA OFISI ZA TMA.

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Ndg. Ludovick Nduhiye amefanya ziara ya kutembelea ofisi za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) zilizopo katika jengo la Ubungo Plaza, Dar es Salaam ikiwa ni moja ya malengo yake ya kuzitambua Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Uchukuzi, kufahamu majukumu ya kiutendaji na kuelewa changamoto zinazowakabili na Mikakati ya kuimarisha Taasisi na utoaji wa huduma. Baada ya taarifa ya utendaji kutoka TMA, Naibu Katibu Mkuu, Uchukuzi aliipongeza TMA kwa kuendelea kuimarisha na kuboresha huduma za haki ya hewa nchini, ikiwemo kuongeza usahihi wa utabiri,  akieleza kuwa yeye ni mmoja wa wadau wa Mamlaka na anafuatilia, kuzingatia na kutumia taarifa za hali ya hewa. 'Kiuekweli taarifa zenu ni nzuri, niwapongeze sana TMA, mimi ni mdau wa taarifa zenu na nimekuwa nikizifuatilia, kuzizingatia na pia kuzitumia, naweza kusema TMA ya sasa si kama ile za zamani." Alisisitiza Ndg. Nduhiye. Aidha, akiwasilisha...

MBUNGE ULENGE NA JITIHADA ANAZOZICHUKUA KUMUUNGA MKONO SAMIA UBORESHAJI ELIMU TANGA

Image
Na Yusuph Mussa,DmNewsOnline  TANGA                         MBUNGE  wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga Mhandisi Mwanaisha Ulenge anasema Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani Machi 19, 2021 amekuwa anafanya kazi kubwa katika kuboresha huduma za jamii ikiwemo elimu, afya na maji. Mhandisi Ulenge anasema Dkt. Rais Samia amefanya yote hayo ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020-2025. Na ilani ya CCM katika kipengele cha elimu, malengo yake ni kuzalisha rasilimali watu bora kwa maendeleo  ya kijamii na kiuchumi. "Hivyo, Serikali imetimiza wajibu wake, ni wajibu wetu  sisi wananchi kuunga mkono jitihada za Serikali ya CCM  kwa kuhakikisha tunaitumia vema miundombinu bora ya elimu ili  jamii yetu  izalishe rasilimali watu bora kwa maendeleo  ya jamii yetu na Taifa letu kwa jumla" anasema Mhandisi Ulenge.  Ulenge ameongeza kuwa katika matokeo ya kidato cha nne...

EMIRATES CELEBRATES JOHANNESBURGS HARDWORKING TEACHERS WITH SPECIAL ADITION BAGS

Image
DmNewOnline Recognising the dedication of South Africa’s hardworking educators, Emirates has gifted 100 teachers with sold-out, limited-edition backpacks from its second ‘Aircrafted by Emirates’ repurposed luggage collection, as part of the airline’s commitment to ‘connecting communities’ by building enduring relationships and making meaningful differences in the destinations it serves. Afzal Parambil, Emirates Regional Manager for Southern Africa said, “Since our first flight to Johannesburg in 1995, we have not only invested in scaling our operations and developing South Africa’s tourism sector but invested in the community too.  Education, much like travel, broadens the mind and brings immeasurable value to society at large. Celebrating these shared values, we wanted to show our appreciation for the teachers in one of Johannesburg’s most impoverished townships. We are proud to enrich the communities we serve.” In the same month as World Teachers Day, the Emirates team based in J...

TASAF ,UNICEF WAZINDUA MPANGO WA STAWISHA MAISHA KUKABILIANA NA MTAPIAMLO KWA KAYA MASIKINI.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline MKURANGA SERIKALI kupitia Mfuko wa  Maendeleo ya Jamii(TASAF)kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo na hasa Shirika la Kimataifa la  Kuhudumia Watoto(UNICEF) wamezindua Mpango wa Stawisha Maisha kwa lengo la kuimarisha hali za lishe kama sehemu ya kukabiliana na changamoto ya utapiamlo kwa kaya masikini ambazo ziko kwenye mpango wa TASAF. Uzinduzi wa Mpango huo umefanyika Oktoba 29,2024 katika Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani  na kuhudhuriwa na viongozi, wadau wa maendeleo pamoja na wananchi ambao ndio walengwa wakuu na Kwa kupitia mpango huo wa Stawisha jamii wananchi watahamasisha kuhusu lishe bora sambamba na kupatiwa mafunzo na kubadilisha uzoefu kupitia katika vikundi ambavvyo wameavianzisha. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo uliofanyika Kijiji cha Mkiu wilayani Mkuranga mkoani humo  uliokwenda sambamba na kukabidhi redio zinazotumia nguvu za jua  kwa vikundi vya walengwa Stawisha Maisha, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF...

WATAALAMU WAZAWA WAPEWE NAFASI KWENYE MIRADI MIKUBWA.

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline  DAR ES SALAAM  MKUU wa Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam Edward Mpogolo amesema serikali imeendelea kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta ya ujenzi wakiwemo wabunifu majengo,wakadiriaji majenzi na wakandarasi ili waweze kupata fursa kwenye miradi mikubwa. Mpogolo amesema hayo  Oktoba 29,2024 alipomwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt .Doto Biteko kwenye ufunguzi  wa mkutano mkuu wa Tano wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB)  uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam . Aidha amewataka wataalamu na kampuni za ndani kuchangamkia fursa na kushiriki katika michakato ya zabuni za miradi mikubwa ili kujijengea uwezo wa kitaalamu na kupunguza utegemezi wa wataalumu kutoka nje kwa kazi za ujenzi na matengenezo. Pia amesema kwamba Serikali imeendelea  kutoa hamasa kwa wataalamu wa ndani kuchangamkia furs...

DIWANI KATA YA ISYESYE AONGOZA WANACHAMA KUSINDIKIZA WAGOMBEA UENYEKITI ZOEZI LA UCHUKUAJI FOMU

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline MBEYA  DIWANI wa kata ya Isyesye(CCM) Jijini Mbeya ,Ibra John  October 28 ,2024 ameongozana na  wanachama wa Chama hizo katika zoezi la uchukuaji  fomu  la  kuwasindikiza wagombea uenyekiti na ujumbe  wa serikali za mitaa  kuchukua fomu  kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa kata .

HOSPITALI YA TAIFA MLOGANZILA YAJIPANGA KUWATIBU WAGONJWA WA KIHARUSI

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline  MLOGANZILA HOSPITAL  ya Taifa ya Muhimbili tawi la Mloganzila katika kukabiliana  na changamoto ya wimbi la kuwepo kwa  idadi kubwa ya wagonjwa wa ubongo,mishipa ya fahamu  na  kiharusi imeamua kutoa elimu  maalumu  kwa wananchi kwa lengo kujikinga na magonjwa hayo. Hospitali hiyo  mbali na kutoa elimu hiyo pia imeweza kutoa huduma mbali mbali za upimaji wa afya wa magonjwa kutoka kwa madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila. Hayo yamebainishwa na Naibu mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila Dkt. Judith  Magandi wakati wa maadhimisho ya siku ya ugonjwa wa kiharusi duniani. Naibu Mkurugenzi huyo ametumia fursa hiyo kuwahimiza  wagonjwa wenye changamoto za kiharusi wajitokeze  ili waweze kupatiwa tiba sahihi kwa wakati kwa lengo la kuepuka madhara zaidi. Dkt. Magandi amesema  kwamba  tatizo la kiharusi ni kubwa na kuongeza kuwa kwa MNH-Mloganz...