AIDAN MLAWA AMPONGEZA RAIS DKT. SAMIA KWA UTENDAJI ULIOTUKUKA



Na Eliasa Ally,DmNewsOline
    IRINGA 

MDAU wa Maendeleo wilaya ya kilolo na Mkurugenzi wa kampuni ya john Galt Hauliers LTD Usafirishaji Mizigo Ndani Nje ya Tanzania.  Aidan Mlawa ampongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kazi kubwa anayoifanya katika Taifa letu la Tanzania 

Mlawa ameyasema hayo mapema wiki hii katika mahojiano na DmNewsonline ambapo amesema Rais Dkt.Samia amefanya Maendeleo makubwa ndani ya uongozi wake amepeleka Maji vijijini, umeme standad gej, Elimu bure, tren imerahisisha wafanyabiashara wanaenda Dodoma kwenda kufanyabiashara kwenda na kurudi na huduma hiyo imewarahisishia wananchi wote 

Mama Samia amefanya mamiradi makubwa ndani ya nchi hii Ambapo sisi wafanyabiasha tukienda nchi za nje tukisema tunatoka nchinij Tanzania wanatamani kuja Kuwekeza Tanzania viwanda,mashamba na vitu mbalimbali 

Mlawa amesema ili Mama Samia aendelee kufanya Mambo makubwa inatakiwa sisi wafanyabiashara na Wananchi inatupasa tulipe Kodi ili Rais tumuunge mkono kuendeleza miradi mikubwa zaidi ya hapa inayoifanya katika Taifa letu 

Watanzania inatupasa kujivunia Rais wetu anaewapenda watanzania wote na amewapa Uhuru wafanyabiashara wote wadogo na wakubwa kufanya Biashara zao Kwa Uhuru na kuwasikiriza changamoto zao na kuzitatua

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025