Posts

Showing posts from July, 2024

DKT. BITEKO AMFARIJI HALIMA MDEE

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akisaini kitabu cha maombolezo kwenye msiba wa Theresia Mdee, Mama mzazi wa Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Halima Mdee leo Julai 31,2024. Dkt. Biteko amefika na kumfariji Mhe. Halima Mdee kufuatia msiba huo uliotokea tarehe 30 Julai, 2024 katika hospitali ya Benjamin Mkapa alipokuwa akipatiwa matibabu Jijini Dodoma.

HEINEKEN BEVERAGE IMEINGIA UBIA NA KAMPUNI YA KITANZANIA MABIBO BIA KWA AJILI YA USAMBAZAJI

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM KAMPUNI ya Heineken Beverage imeingia makubaliano na  kampuni ya kitanzania Mabibo bia kwa ajili ya usambazaji wa bia ya Windhoek inayotengenezwa  nchini Namibia. Akizungumza na waandishi wa habari Leo julai 31,2024  Meneja Mkazi wa Kampuni ya Heineken Obabiyi Fagade amesema lengo la kuingia ushirikiano huo ni mkakati mahususi wa kusaidia biashara za ndani na ukuaji wa uchumi  nchini Tanzania na kupata fursa za ukuaji katika ya kusini mwa Afrika "Ushirikiano huo na Mabibo bia ,wines na spirits ni kufungua ukurasa  mpya kwa kuunganisha utaaalamu wetu wa Kimataifa Kama Heineken na ujuzi mkubwa walionao katika soko la ndani,tuna uhakika katika uwezo wetu wa kuwasilisha bidhaaa na huduma za kipekeee kwa watej wetu Tanzania";,amesema . Ameongeza kuwa Heineken imedhamiria kutoa  huduma za kipekeee kupitia vinywaji vyenje ubora wa hali ya juu ambavyo vinakizi ladha ya watumiaji. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya M...

BOT. YAJA NA MPANGO WA KUPUNGUZA KUTUMA PESA MTANDAONI.

Image
Na Mwandishi wetu, DmNewsOnline DAR ES SALAAM KATIKA jitihada ya kuwawezesha  Watanzania maskini kushiriki katika ujenzi wa Taifa na kunufaika na uchumi wa kijiditali, Benki Kuu ya Tanzania imebuni mpango wa kutuma fedha mtandaoni ambao gharama zake zitakuwa chini  ya zile zinazotozwa na kampuni za simu nchini na wadau wengine. Gavana wa Benki Kuu (BoT), Bw Emmanuel Tutuba, ameeleza kuwepo kwa mpango huo wakati akiongea na waandishi wa habari ambao walitaka aeleze kidogo umuhimu wa Mpango Mkakati wa  Uchumi wa  Kidijitali Tanzania wa miaka 10 (Tanzania Digital Economy Strategic Framework  2024-2034).   Amesema Benki Kuu hivi karibuni imezindua mpango ambao ni rahisi  kwa mtu kutoa fedha kutoka akaunti yake, akapitisha fedha hiyo katika mpango huo unaoitwa TIPS (Tanzania Instant Payment System) ambao  umeunganisha wadau mbali mbali ili malipo yafanyike kwa urahisi; yaani mtu kutokea benki yake aweze  kumlipa mtu kwenye benki nyingine au kampun...

SEKTA BINAFSI YAPEWA KIPAUMBELE KUPITIA TRENI YA SGR

Image
Na  Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM SERIKALI  kupitia  Wizara  ya Uchukuzi  imetoa Kipaumbele kwa Sekta  binafsi katika kushirikiana kwenye  uwekezaji  wa treni ya kisasa SGR ili kuleta maendeleo  ya kiuchumi nchini. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam  Waziri wa Uchukuzi  Profesa Makame  Mbarawa  amesema kuwa  Shirika la Reli Tanzania ( TRC )kwa kushirikiana na wizara ya uchukuzi linawakaribisha  sekta ambazo sio za kiserikali   katika kuweza  kuongeza chachu ya maendeleo ya Treni ya kisasa ya SGR. “Tumejenga reli hii   kwa  kuweza  kurahisha biashara  mbalimbali  nchini kwetu  Tanzania kwani  ni  nchi pekee ambayo tunatumia mtandao  mkubwa wa reli ya kisasa yenye kilomita 720 na kupitia reli hii mizigo ndiyo itakayoleta faida kubwa na kukuza pato la taifa  huku wasafiri wa kawaida  wakiwa  na muitikio ...

MTEMVU ACHANJA MBUNGA KATA KWA KATA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline KIBAMBA  MBUNGE  wa Jimbo la Kibamba Issa Mtemvu ameingilia kati na  kumaliza sakata la mvutano na mgogoro wa mradi wa ujenzi wa zahanati katika mtaa wa gogoni kata ya Kibamba ambao umedumu kwa pindi kirefu bila ya kuanza kujengwa. Kukwama kwa mradi huo umeleta hali ya sintofahamu kwa wananchi,viongozi wa serikali,na wa chama cha mapinduzi  kutokana na kusuasua kwa kwa kipindi cha muda mrefu  licha ya kuwepo kwa eneo lililotolewa na serikali. Kutokana na hali hiyo imemlazimu  Mhe.Mtemvu kuamua kufanya ziara yake ya kikazi   yenye lengo la kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo  inayoendelea  kutekelezwa  na ile iliyokwama ili kuweza kuitafutia ufumbuzi wa kudumu. Mtemvu alibainisha kwamba lengo la Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kuboresha huduma ya afya ili wananchi waweze kuondokana na changamoto za matibabu. "Nipo katika ziara yangu ya kikazi lakini lengo lake kubwa ni kutembelea n...

ZIARA YA BALOZI NCHIMBI YAFYEKA ACT, CUF NA CHADEMA KUSINI

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline LINDI  ZIARA  ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, inayoendelea katika mikoa ya Kusini, akianzia Mtwara na sasa yuko Lindi, imewahamisha viongozi waandamizi wa vyama vya ACT Wazalendo, CUF na Chadema walioamua kujiunga CCM leo, wakisindikizwa na mamia ya wanachama waliorejesha kadi zao za vyama vya zamani kwa kasi kubwa kwenye mkutano wa hadhara.  Katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Mpilipili, Lindi mjini, ukiwa ni mwendelezo wa ziara ya Balozi Nchimbi, amewapokea viongozi hao waandamizi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Mkoa wa Lindi na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Mchinga Ndugu Hamidu Bobali. Wengine ni  viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Wanawake wa ACT Wazalendo Lindi Mjini Bi. Hawa Kipara, Meneja Kampeni wa Wabunge ACT Wazalendo Lindi na aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana CUF Lindi Issa Sapanga, Katibu wa ACT Wazalendo Mkoa wa Pwani, Mwenyek...

WHI NA MKANDARASI SHADONG HI-SPEE GROUP WATIA SAINI MKATABA UJENZI WA NYUMBA 101.

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM MKURUGENZI Mtendaji wa Watumishi Housing Investments (WHI) Dkt.Fred Msemwa amesaini mkataba wa ujenzi wa nyumba 101 zitakazojengwa eneo la Mikocheni Regent Estate Jijini Dar es Salaam. Mkataba huo ni baina ya WHI na Mkandarasi Shadong Hi-Speed Group ambapo utiaji Saini umefanyika leo Julai 30,2024 katika Ofisi za WHI jijini Dar es salaam Dkt.Msemwa amesema ujenzi huo utaanza mwezi Agosti 2024 na unahusu ujenzi wa jengo la ghorofa 12 lenye nyumba 101 ambapo Kila mnunuzi atamilikishwa nyumba atakayonunua ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Makazi kwa Watumishi wa Umma. Aidha amesema WHI tayari imejenga nyumba 1,003 katika mikoa 19 nchini Tanzania na  sehemu ya nyumba 218 zitajengwa katika mikoa ya Dodoma,Lindi,Mtwara,Singida,Pwani na Ruvuma katika mwaka wa fedha 2024/2025. "Ujenzi wa mradi huu wa nyumba 101 utagharimu kiasi Cha shilingi Bilioni 18.6 na ujenzi wake utafanyika kwa kipindi cha miezi 18.Nyumba hizi zitauzwa kwa utara...

KATIBU MKUU CCM DKT NCHIMBI KUWASILI LINDI LEO ,KUHUTUBIA WANANCHI VIWANJA VYA MLIPILI.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline LINDI KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), DKt. Emmanuel Nchimbi leo alasiri anatarajiwa kuzungumza na wananchi wa Lindi kwenye mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika Uwanja wa Mpilipili, Mjini Lindi. Balozi Nchimbi na msafara wake, atapokelewa rasmi asubuhi ya leo katika Ofisi za CCM za Mkoa huo, ambapo atafanya kikao na Kamati ya siasa na baadaye mkutano wa ndani wa makundi mbalimbali.  Lengo la ziara hiyo ni  Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki Taarifa zao na kujiandikisha katika Daftari la Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Novemba mwaka huu. Katika ziara hii Dkt Nchimbi kabla ya kuingia mkoani Lindi, amemaliza ziara ya siku mbili mkoani Mtwara, ambapo ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Is...

UVCCM,DAS KIBAHA WATUA KITUO CHA AFYA MKOANI KUFANYA USAFI NA KUCHANGIA DAMU

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline KIBAHA    OFISI ya Wilaya ya Kibaha kwa kushirikiana na Umoja wa vijana (UVCCM)  Kibaha mjini katika kutekeleza agizo la serikali la kufanya  usafi wa mazingira ifikapo kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi  imeamua kutambulisha rasmi  Club ya Jogging pamoja na  kufanya  mazoezi kwa ajili ya kujenga afya zao na ili kuweza kujikinga na kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza. Utambulisho huo wa Jogging inayotambulika kwa jina la Kibaha Fitness Club umekwenda sambamba na zoezi la ufanyaji wa  usafi katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Wilaya ya Kibaha pamoja na uchangiaji wa damu kwa ajili ya kuweza kuwasaidia wagonjwa mbali mbali wenye uhitaji hususan wakinamama wajawazito. Akizungumza  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibaha  Moses Magogwa amesema kwamba wameamua kuungana na  vijana wa UVCCM  kufanya usafi wa mazingira ikiwa ikiwa ni moja ya utekelezaji wa agizo la s...

RAIS SAMIA ARIDHIA KINANA KUJIUZULU CCM

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline  Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) amejiuzulu wadhifa huo baada ya Mwenyekiti wa Chama hicho na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuridhia ombi lake. Hayo yamebainishwa katika taarifa iliyotolewa leo Julai 29, 2024 na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makala akisema Kinana ameandika barua ya kuomba kupumzika. Katika majibu yake Mwenyekiti wa CCM Samia amesema "Ni kweli nilipokuomba utusaidie kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti nilikuahidi utakaa muda mfupi kama ulivyoomba, na kwa kweli nilipenda uendelee kutusaidia lakini kwa kuwa umeomba sana na ahadi ni deni nalazimika kwa moyo mzito kuridhia kujiuzulu kwako." Imesema taarifa hiyo. Pia Samia amesisitiza kuwa Chama kitaendelea kutumia uzoefu na maarifa ya Kinana kila itakapohitajika. 

NCHIMBI AWAPONGEZA MTWARA VIJIJINI UTEKELEZAJI ILANI YA CCM

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  MTWARA KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiambatana na Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, ameendelea na ziara yake ya mikoa miwili ya Kusini, Lindi na Mtwara leo tarehe 29 Julai 2024 amepata fursa ya kuzungumza na Wananchi wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Kata ya Mpapura.  Akiwa hapo Mpapura, Balozi Nchimbi amesema pamoja na kwamba jimbo hilo linaongozwa na mbunge asiyekuwa wa CCM, lakini Ilani ya Uchaguzi inayotekelezwa ni ya CCM, ambapo aliwapongeza wanachama na viongozi wa CCM na wananchi, kwa kushirikiana na Serikali ya CCM, kuhakikisha ilani hiyo inatekelezwa kwa kiwango cha juu.  Ameongeza kusema kuwa hilo limefanikiwa kwa sababu Mbunge wa CCM Jimbo la Nanyamba, Mhe Abdallah Chikota anafanya kazi pia ya kuwa kaimu mbunge kuwawakilisha na kuwasemea wananchi wa Mtwara Vijijini.  “Hapa hakika kazi Imefanyika nafikiri mmeona sasa kazi kwenu wakati ukifika inadili mbadilike kwani...

SERIKALI KUZINDUA SERA MPYA YA BIASHARA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline Serikali inatarajia kuzindua Sera mpya ya Taifa ya  Biashara  ya 2003 Toleo la 2023 yenye dhamira ya kuweka mfumo  na mkakati madhubuti unaolenga kuboresha mazingira ya biashara, kuongeza ajira, Pato la Taifa, ukuaji wa kiuchumi na kuboresha ustawi wa wananchi. Sera  hiyo mpya toleo la 2023 imeoanisha Sera na kanuni za biashara na Sera zinazohusiana na masuala ya kibiashara, kuondoka mgongano wa kisheria, mgawanyo wa majukunu ya kitaasisi, kuimarisha miundombinu ya masoko na biashara, kupunguzwa muda na gharama za ufanyaji biashara, kuwezesha biashara mtandao, biashara ya huduma, usimamizi wa ushindani halali wa kibiashara na kumlinda mlaji. Hayo yamesemwa na Waziri wa  Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo Julai 28, 2024 Dar es Salaam alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa Sera hiyo utakaofanyika Julai 30, 2024 jijini Dar es Salaam. Aidha amebainisha kuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Sera hiyo inayoon...