SEKTA BINAFSI YAPEWA KIPAUMBELE KUPITIA TRENI YA SGR



Na  Angelina Mganga,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM

SERIKALI  kupitia  Wizara  ya Uchukuzi  imetoa Kipaumbele kwa Sekta  binafsi katika kushirikiana kwenye  uwekezaji  wa treni ya kisasa SGR ili kuleta maendeleo  ya kiuchumi nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam  Waziri wa Uchukuzi  Profesa Makame  Mbarawa  amesema kuwa  Shirika la Reli Tanzania ( TRC )kwa kushirikiana na wizara ya uchukuzi linawakaribisha  sekta ambazo sio za kiserikali   katika kuweza  kuongeza chachu ya maendeleo ya Treni ya kisasa ya SGR.

“Tumejenga reli hii   kwa  kuweza  kurahisha biashara  mbalimbali  nchini kwetu  Tanzania kwani  ni  nchi pekee ambayo tunatumia mtandao  mkubwa wa reli ya kisasa yenye kilomita 720 na kupitia reli hii mizigo ndiyo itakayoleta faida kubwa na kukuza pato la taifa  huku wasafiri wa kawaida  wakiwa  na muitikio mkubwa wa kutumia treni hiyo .

Aidha   serikali  imeweza kutumia Dolla Milioni 3.138   kukamilisha ujenzi wa reli huku Shilingi Trillion 1.3 zimetumika kununua vitendea kazi vikiwemo mabehewa 89, seti 10 za vichwa vya treni ya mchongoko na vichwa 19  vya treni ya umeme”.amesema Profesa  Mbarawa.

Tumeona wananchi wengi kutoka maeneo jirani  wamefurahishwa na huduma hizo hivyo  wanatumia usafiri huo wa treni  katika kukuza na kuendeleza uchumi kutoka kwenye serikali yetu.

Hata hivyo   Profesa Mbarawa ameongeza kuwa kupitia uzinduzi  huo wa treni za kisasa SGR kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma  unaenda kufanyika  Jijini Dodoma Agosti 1,2024  huku mgeni rasmi wa uzinduzi  huo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt . Samia Suluhu Hassan .

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025