HEINEKEN BEVERAGE IMEINGIA UBIA NA KAMPUNI YA KITANZANIA MABIBO BIA KWA AJILI YA USAMBAZAJI




Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Heineken Beverage imeingia makubaliano na 
kampuni ya kitanzania Mabibo bia kwa ajili ya usambazaji wa bia ya Windhoek inayotengenezwa  nchini Namibia.

Akizungumza na waandishi wa habari Leo julai 31,2024  Meneja Mkazi wa Kampuni ya Heineken Obabiyi Fagade amesema lengo la kuingia ushirikiano huo ni mkakati mahususi wa kusaidia biashara za ndani na ukuaji wa uchumi  nchini Tanzania na kupata fursa za ukuaji katika ya kusini mwa Afrika

"Ushirikiano huo na Mabibo bia ,wines na spirits ni kufungua ukurasa  mpya kwa kuunganisha utaaalamu wetu wa Kimataifa Kama Heineken na ujuzi mkubwa walionao katika soko la ndani,tuna uhakika katika uwezo wetu wa kuwasilisha bidhaaa na huduma za kipekeee kwa watej wetu Tanzania";,amesema .

Ameongeza kuwa Heineken imedhamiria kutoa  huduma za kipekeee kupitia vinywaji vyenje ubora wa hali ya juu ambavyo vinakizi ladha ya watumiaji.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Bia Jerome Rugilamalila  amesema  mkataba huo wa kibiashara umekuja baada ya kampuni ya Mabibo na Namibia Breweries kukubalina kuvunja mkataba walioingia mwak 2008.



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025