Posts

Showing posts from April, 2024

KAMPUNI YA ORYX GESI TANZANIA YAFANYA KUFURU KWA WAHARIRI NA WAANDISHI WA HABARI ,WAGAWA MITUNGI YA GESI NA MAJIKO YAKE.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  DAR ES SALAAM KAMPUNI ya Oryx Gesi imekabidhi mitungi ya gesi ya kilo 15 na majiko yake Kwa wahariri ,waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya Mpango wake wa kuhamasisha matumisi ya Nishati safi ya Kupikia  Kwa watanzania Akizungumza katika hafla fupi ya ugawaji wa mitungi hiyo  iliyofanyika Leo April 30 ,2024 Kwenye Kiwanda cha Kampuni kilichopo  wilayani kigamboni jijini Dar es salaam mkurugenzi mkuu BenoIte Araman Oryx Gas Tanzania wanauwezo wa kusambaza na kutoa Gas Tanzania bara na visiwani kwa wakati, muda wowote na sehem zote. "Kwetu Oryx Gesi tukio hili tumelipa uzito mkubwa na hii inatokana na umuhimu wenu katika jamii yetu, kwetu sisi Oryx vyombo vya habari vimekuwa daraja na kiunganishi kikubwa cha kufikisha taarifa zinazohusiana na nishati safi ya kupikia na hasa inayotokana na gesi ya oryx kwa jamii."Amesema mkurugenzi Araman  Nakuongeza kuwa "Sote tunafahamu Serikali yetu ya Awamu ya Sit...

'RUWASA- KAYA 796 KATA YA FUKAYOSI KUONDOKANA NA KERO YA MAJI IFIKAPO MEI 11 2024

Image
Na Victor Masangu DmNewsOnline,Bagamoyo  WANANCHI  3666 katika kijiji cha Kidomole  na vitongoji vyake mbali mbali vilivyopo katika  kata ya Fukayosi  Wilayani Bgamoyo Mkoa wa Pwani wanatarajia kuondokana na changamoto ya usumbufu wa majii fikapo mwezi Mei mwaka huu baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji ambao utakuwa ni mkomboz mkubwa kwa wananchi hao. Hayo yamebainishwa na  Meneja wa wakala wa Usambazaji wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Wilaya ya Bagamoyo  James kionaumela wakati akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za Mwenge  wa Uhuru  kitaifa ndugu  Godfrey Mnzava kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo ambapo alisema kwa sasa upo katika hatua za mwisho kwa ajili ya upanuzi. Meneja huyo alibainisha kwamba unatekelzwa chini ya mkandarasi mzawa AM&Partiner Limeted na Building Contractors kutoka jijini Dar es Salaam na kwamba kwa mujibu wa mkataba huo mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Mei 11 mwaka huu. Amefa...

KUNDI LINGINE LENYE WANANCHI 564 LAHAMA HIFADHI YA NGORONGORO.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline  NGORONGORO ZOEZI la wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kujiandikisha na kuhama kwa hiari limepamba moto ambapo leo tarehe 28 Aprili, 2024 jumla ya Kaya 105 zenye wananchi 564 na mifugo 1,540 zimehama katika hifadhi ya Ngorongoro kwenda Kijiji cha Msomera, Simanjiro, Meatu na Monduli. Kwa mujibu wa Meneja mradi wa kuhamisha wananchi wanaojiandikisha kuhama kwa hiari, Afisa Uhifadhi Mkuu Florah Assey, kati ya kaya hizo 105 zenye wananchi 564 wanaohama,  kaya 96 zenye watu 520 na mifugo 1,424 zinahamia Kijiji cha Msomera huku kaya 9 zenye watu 44 na mifugo 116 zikihamia wilaya za Simanjiro mkoani Manyara, Meatu Mkoani Simiyu, Monduli mkoani Arusha na Dakawa Mkoani Morogoro. Assey amebainisha kuwa zoezi la kuelimisha, kuandikisha na kuthaminisha mali za wananchi linaendelea ndani ya hifadhi hiyob ambapo kila kaya inayojiandikisha mkuu wa kaya na wategemezi wake hukabidhiwa nyumba yenye vyumba vitatu katika kiwanja chenye ukubwa wa eka...

TIMU YA WIZARA YA MALISILI NA UTALII YATOA MISAADA KWA WAHITAJI ARUSHA

Image
Na John Bera Dm,NewsOnline    ARUSHA  TIMU  ya michezo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii ikiongozwa na Mwenyekiti wa Timu hiyo, Getrude Kassara pamoja na viongozi mbalimbali wa Timu hiyo wamekabidhi  misaada ya hisani kwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mei Mosi, Bi. Itika Mwankenja kwa ajili ya  kuipeleka kwa wahitaji  waliopo Mkoani Arusha ili iweze kuwasaidia. Timu hii imedhihirisha ukarimu mkubwa kwa jamii kwa kuwasaidia watu wanaohitaji. Hatua hii ni mfano mzuri wa umoja na mshikamano katika kusaidia jamii kwa ujumla Aidha, Wizara ya Maliasili na Utalii inajivunia kuwa na timu yenye moyo wa kujitolea ambayo  mbali na kuhamasisha utalii wa michezo pia, inarudisha kwa  jamii kwa namna moja au nyingine

UVCCM KIBAHA MJINI YAMPA HEKO MAMA KOKA KWA KUWAPAMBANIA NA MISAADA

Image
Na Victor Masangu,DmnewsOnline Kibaha JUMUIYA  ya Umoja wa vijana ya Chama cha mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kibaha mji umempongeza kwa dhati mke wa Mbunge wa  Jimbo la Kibaha mji Selina Koka kwa kuona umuhimu wa kuwasapoti vijana kwa kutoa  msaada wa  mahitaji na vitu  mbali mbali ikiwa ni utekelezaji wa ahadi zake alizozitoa  kwa vijana. Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kibaha mjini Gamalu Makona wakati wa halfa fupi ya kukabidhiwa baadhi ya mahitaji na vitu mbali mbali kwa ajili ya kuwasaidia vijana wa hamasa ambao wapo katika mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na  kuupokea Mwenge wa uhuru. Aidha Katibu huyo amesema kwamba Mama Koka amekuwa mstari wa mbele katika kusaidia mambo mbali mbali katika jumuiya ya vijana katika Jimbo la Kibaha mji. Ameongeza kwamba Mama Koka amewashika mkono na kuwapatia msaada wa vyakula mbali mbali,sambamba na mabati viti meza kwa ajili ya ujenzi wa banda ambalo litakuwa linatumika kukutana vijana wa uvccm ...

JENERALI MABEYO AWAVISHA VYEO MAKAMISHNA WAPYA NGORONGORO

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline    MWENYEKITI  wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu) Aprili,29, 2024 amewavisha vyeo maafisa Uhifadhi wakuu waliopandishwa vyeo hivi karibuni katika tukio lililofanyika ofisi za Makao makuu ya NCAA Karatu Mkoani Arusha. Waliovishwa vyeo ni Afisa Uhifadhi Mkuu Lilian Magoma ambaye amepandishwa na kuvishwa cheo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango, tathmini na ufuatiliaji na Afisa Uhifadhi Mwandamizi wa Rasilimali watu Salma Chisonga aliyepandishwa cheo  amevishwa cheo kuwa Kamishna msaidizi Mwandamizi wa uhifadhi, Rasilimali watu na Utawala. Jenerali Mabeyo amewataka makamishna wapya kufanya kazi kwa kujituma na kuzingatia viapo vyao katika misingi ya uzalendo, maadili ya utumishi, ushirikiano, maarifa na bidii ya kazi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

MKOA WA PWANI YATUMIA TRILIONI 8.5 KUTEKELEZA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE.

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline  KIBAHA MBIO za Mwenge wa Uhuru umewasili leo rasmi mkoani Pwani ukitokea Mkoani Morogoro ambapo umekabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge ambapo utatembelea na kuzindua miradi mbali mbali ya maendeleo mkoani humo. Akipokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima  amesema kwamba katika mbio hizo mwenge huo utatembelea jumla ya miradi 126. Kunenge amebainisha kwamba mbio za Mwenge huo wa uhuru kwa mwaka huu  utakimbizwa katika Halmashauri tisa zilizopo katika Wilaya saba  ambapo jumla ya kilometa 1,225.3 zitakimbizwa katika maeneo mbali mbali.  Kunenge amefafanua kwamba kati ya miradi hiyo miradi 18 itawekewa mawe ya msingi,miradi 22 itazinduliwa na miradi ipatayo 86 itakaguliwa. Aidha Kunenge amesema kuwa miradi hiyo itagharimu  kiasi cha shilingi Trilioni 8.536  ambapo serikali kuu imechangia bilioni 13.6,Halmashauri za wilaya shilingi bilioni 2.3 nguvu za wananchi na wawekezaji tri...

ULEGA AHIMIZA UWEKEZAJI WA MITAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega  amesema sekta za mifugo na uvuvi zinaweza kuwa na tija kubwa zaidi kama taasisi za kifedha zitaendelea kuwekeza mitaji katika shughuli za mifugo na uvuvi ili ziweze kuzalisha kwa tija na hivyo kuchangia vyema kwenye pato la taifa. Ulega amesema hayo wakati akifafanua baadhi ya hoja za wadau wa Kongamano la Uwekezaji la CRDB lililopewa jina la “Uwekezaji Day 2024”linalofanyika jijini Dar es Salaam leo 2024.  Amesema sekta za mifugo na uvuvi zinaweza kuwa na  tija kubwa katika uchumi wa taifa hivyo ni muhimu taasisi za kifedha ikiwemo CRDB kuendelea kuwekeza mitaji ili kuinua wadau wanaojishughulisha na sekta hizo. “Nawapongeza CRDB kwa kuaandaa Kongamano hili kubwa la uwekezaji day, ombi langu kwenu, jukwaa hili liwe chachu ya kubadili sekta hizi za uzalishaji kwa kuongeza mitaji ili kuchechemua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla”, amesema Akizungumza katika mahojiano maalumu...