MKOA WA PWANI YATUMIA TRILIONI 8.5 KUTEKELEZA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE.




Na Victor Masangu,DmNewsOnline  KIBAHA

MBIO za Mwenge wa Uhuru umewasili leo rasmi mkoani Pwani ukitokea Mkoani Morogoro ambapo umekabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge ambapo utatembelea na kuzindua miradi mbali mbali ya maendeleo mkoani humo.

Akipokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima  amesema kwamba katika mbio hizo mwenge huo utatembelea jumla ya miradi 126.

Kunenge amebainisha kwamba mbio za Mwenge huo wa uhuru kwa mwaka huu  utakimbizwa katika Halmashauri tisa zilizopo katika Wilaya saba  ambapo jumla ya kilometa 1,225.3 zitakimbizwa katika maeneo mbali mbali. 

Kunenge amefafanua kwamba kati ya miradi hiyo miradi 18 itawekewa mawe ya msingi,miradi 22 itazinduliwa na miradi ipatayo 86 itakaguliwa.

Aidha Kunenge amesema kuwa miradi hiyo itagharimu  kiasi cha shilingi Trilioni 8.536  ambapo serikali kuu imechangia bilioni 13.6,Halmashauri za wilaya shilingi bilioni 2.3 nguvu za wananchi na wawekezaji trilioni 8.5 na wadau wa maendeleo bilioni 14.6.

Pia amemshukuru Rais wa awamu ya sita kwa kuweka mazingira bora kwa ustawi na ufanisi zaidi katika sekta binafsi nchini.

Pia Kunenge katika hatua nyingine alisema kwamba katika kupambana na janga la ukimwi wameendelea kupambana kwa kutoa elimu ya upimaji wa wenza.

Kadhalika ameongeza katika kupambana na dawa za kulevya wameendelea kuimarisha mapambano kwa kubadilisha fikra,hisia na tabia.

Awali kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Godfrey Mnzava alizitaka halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaandaa nyaraka zote za miradi ya maendeleo.



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025