Posts

Showing posts from October, 2025

Article 19 kushirikiana na JOWUTA kusaidia wanahabari nchini

Image
  Mwandishi wetu DmNewsOnline                  Nairobi SHIRIKA  la kimataifa la Article 19, Afrika ya Mashariki, limeahidi kushirikiana na chama cha wafanyakazi katika vyombo vya habari Tanzania(JOWUTA) kusaidia kuwajengea uwezo wanahabari katika masuala ya utetezi wa sheria za habari, haki za wanahabari na ukatili kwa wanahabari wanawake. Makubaliano ya ushirikiano huo, yamefanyika jijini Nairobi, baina ya JOWUTA na Article 19, mara baada ya mkutano wa taasisi za vyombo vya habari katika nchi za Afrika ya Mashariki,kujadili masuala ya uhuru wa vyombo vya habari, ushirikiano na utetezi wa wanahabari. Naibu Mkurugenzi wa Article 19, Patrick Mutahi akizungumza na Mwenyekiti wa JOWUTA, Mussa Juma alisema  taasisi hiyo inatambua changamato za sekta ya habari katika nchi za Afrika ya Mashariki ikiwepo Tanzania na itafanyakazi na JOWUTA. Mutahi amesema, kutokana na changamoto hizo, Article 19 kwa kushirikiana na wahisani wake kadhaa ...

KIBONDE AWATAKA WATANZANIA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline               Chato,Geita MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Makini, Coaster Kibonde amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 ili waweze kutimiza haki Yao ya kikatiba . Hayo ameyabainisha Oktoba 17,2025 alipotembelea nyumbani kwa Hayati John Pombe Magufuli Chato Mkoani Geita na kupata fursa ya kuzuru kaburi la hayati Magufuli. Mgombea Kibonde ameambatana na mgombea Mweza , Azza Haji Suleiman na Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha Makini,Ameir Hasani Ameiri na viongozi wengine wa Chama akiwemo Makamu Mwenyekiti Bara,Gress Boniface Ngonyani,Katibu mwenezi Taifa Fahim Nassor na Naibu Katibu Mwenezi Taifa, Ramadhani Said Bambo pamoja na Mkuu wa Idara ya Urafiti,Sera na Nyaraka, John January Mboya mkoa wa Geita ambao ni mkoa wa 20 toka aanze kampeni za kuwaomba kura watanzania . "Niwaombe Watanzania wenzangu tujitokeze kwa wingi tukapige kura kwa amani na kuwaasa watanz...

LUFEZUWA AWATAKA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI

Image
   Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline           DAR ES SALAAM  MGOMBEA Ubunge Jimbo la Temeke kupitia chama Cha National Labour Party (TLP),Mohamed Shabani Lufezuwa amewataka watanzania kudumisha amani,kwani amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani Hayo ameyabainisha na mwandishi katika mahojiano maalum na mwandishi wa Dmnews Jijini Dar es Salaam amesema kwamba "niwaombe watanzania wenzangu siku zimeisha tunakaribia kwenda kupiga kura bado siku chache kwahiyo tukapige kura kwa amani na tukawachague wagombea wa TLP kwa nafasi ya Urais,Ubunge na Udiwani ili tuwaletee maendeleo watanzania Mgombea Lufezuwa amebainisha vipaumbele kwa maendeleo ya Jimbo la Temeke ambavyo ni elimu,uchumi na huduma za jamii  . Amesema endapo atapata ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo Hilo nitahakikisha kwamba uchumi unakuwa Kwa Kasi kwa wananchi wa Jimbo la Temeke "Niwaombe sana ,Watanzania wenzangu,mkapige kura kwa amanu na kukiletea ushindi wa kishindo Ch...

SERIKALI ITAENDELEA KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI-MAJALIWA

Image
Na Mwandishi wetu,DmMewsOnline             Dar es Salaam  ▪️Asema Wajasiriamali ni nguzo katika kukuza uchumi_   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa makundi mbalimbali ya kijamii kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kijamii.   Amesema Serikali inafanya hivyo kwa kutambua kuwa kundi la Wajasiriamali ni muhimu na nguzo katika katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia shughuli zao.   Amesema hayo leo Ijumaa (Oktoba 17, 2025) wakati wa mkutano wake na makundi mbalimbali ya Wajasiriamali wa jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini humo.   “Ninyi no watu muhimu sana kwenye uchumi wa nchi hii, na mmetoa mchango mkubwa sana kwenye uchumi wa nchi hii, nataka niwahakikishie Serikali hii inanufaika nawe na ndio maana Serikali inaendelea kuwathamini na inapanga mipango mbalimbali juu yenu, Endeleeni kuim...

WANANCHI WATAHADHARIWA NA VIVIMBE VINAVYOJITOKEZA KWENYE MWILI.

Image
  Timothy Marko DmNews online            DAR ES SALAAM. WANANCHI wametakiwa  kufanya Uchunguzi wa kiafya Mara kwa Mara Juu ya Kuvimba unaojitokeza kwenye Mili yao, ilikuweza kuondokana na Tatizo la Ugonjwa wa Saratani. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam katika Semina ilioyowakutanisha  Waandishi wa habari na  wahariri wa Vyombo vya Habari Meneja Huduma za Uchunguzi wa Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt.Maguhwa Stephano amesema Takwimu za Taasisi hiyo zilizofanywa 2024 zilionesha kuwa kati ya Wagonjwa 900walihudhuria Taasisi hiyo walibainika kuwa na Ugonjwa wa Saratani huku kati yao 100 walibainika kuwa na Dalili za Ugonjwa huo watano kati yao walikuwa Wanawaume Ambapo Wanaume hao, walibainika kuwa kuwa Saratani ya vivimbe kwenye matiti. "Tunawahimiza Wananchi kufanya Uchunguzi wa Uvimbe wowote unaojitokeza kwenye mwili  kwani Ni chanzo kikuu cha Saratani"Amesema Meneja Huduma za Uchunguzi wa S...

DKT. SAMIA AMWAGA NEEMA NIDA.

Image
 Na ShusÄ¥u Joel,DmNewsonline                        DAR  SERIKALI imeipatia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Magari Mapya 140 kwa lengo la kuboresha zaidi utendaji  kazi wa Mamlaka hiyo ,Hatua ambayo imepokelewa kwa mikono miwili na hasa ikizingatiwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa zilizokuwa zikiikabili Mamlaka hiyo ni uhaba mkubwa wa magari Hatua hii ni utekelezaji wa ahadi za serikali ya awamu ya sita katika kuboresha huduma zake katika nyanja mbalimbali ikiwemo usajili na utambuzi wa watu nchini  unaotekelezwa na NIDA , na inaonyesha dhamira ya dhati ya serikali ya kusogeza huduma zake kwa wananchi.  Aidha hatua hii ya serikali kuipatia NIDA magari hayo inalenga pia kusaidia,kuimarisha  utekelezaji wa maono ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuhusu jamii namba kwa kuanza kusajili watoto kuanzia wanapozaliwa na kupewa utambulisho wa Taifa unaojulikana kama Jamii namba ili  kuwaw...

GEKULA:WANANCHI NICHAGUENI NIWALETEE MAENDELEO MAJOHE.

Image
Mgombea Udiwani kata ya Majohe katikati aliyevaa shaeti la kijani Julius Gekula Warioba akiwasili katika mtaa wa rada Manispaa ya ilala . ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Octoba 29,mwaka huu nchi nzima . Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                  DAR ES SALAAM MGOMBEA Udiwani kata ya Majohe Halmashauri ya Ilala jijini Dar es salaam  Julius Gekula Warioba  amewaeleza wananchi wa kata hiyo Umuhimu wa kumchagua kuwa diwani wao na kwamba akiwa katika nafasi za ujumbe wa Serikali ya mtaa na Ofisa mtendaji wa mtaa huko nyuma alifanya kazi kwa uadilifu mkubwa.  Amesema anaishukuru Chama chake Cha Mapinduzi CCM na wanaccm wa kata ya majohe kuweza kumwamini na kukubari kupeperusha bendera ya Chama kwa nafasi ya Udiwani hivyo jukumu alililonalo huko mbele baada ya kuchaguliwa Octoba 29,mwaka huu. Nikuwatumikia wananchi hao kwa uweza wake wote. Gekula ameyasema hayo leo Octoba 16 ,2025 k...

TOSCI YAWAASA WAKULIMA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU

Image
    Na Mwandishi wetu,TANGA TAASISI  ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI ) imeendelea kuwaasa wakulima kujisajili kwenye mfumo wa Ruzuku wa Mbegu. Kauli hiyo imetolewa leo Octoba ,16,2025 na Mkurugenzi wa Tathimini na majaribio kutoka TOSCI Matenga M. Swai kwenye viwanja vya Usagara Jijini Tanga wakati wa kilele Cha Maadhimisho ya siku ya chakula Duniani yenye kauli mbiu ya Tuungane pamoja kupata chakula Bora kwa Maisha Bora ya Baadae. Matenga amesema wakulima na Watanzania wote washirikiane kwa pamoja ili wapate Mbegu Bora  na wazingatie Ubora kwa maana hiyo wanunue Mbegu zilizopo kwenye vifungashio na waakikishe wanapewa risti. Amesema TOSCI imeanzisha mfumo wa usajili Mtandao yaani Online.ambao unasajili kwa mfumo wa Ruzuku kuanzia ngazi ya Wilaya Ameongeza kuwa  majukumu ya TOSCI ni kushugulikia maswala ya Mbegu kukagua maghala hayo yanafanywa kwa kushirikiana na Maafisa ugani waliopewa mafunzo na TOSCI. Ameongeza kuwa wanapita kwa wauzaji yaani madu...

HAMOUD JUMAA:DKT SAMIA AMEILETEA NCHI MAENDELEO .

Image
Mgombea ubunge Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa akiwa katika Kata ya Kwala kwa ajili ya kufanya kampeni za kuomba ridhaa Wananchi wamchague Oktoba 29 mwaka huu Na Gustaphu Haule, DmNewsonline                    PWANI MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa ( Mzee Sambusa ) amemmwagia sifa Rais  Dkt.Samia Suluhu Hassan kutokana na ushujaa wake wa kuiletea nchi maendeleo. Jumaa amesema CCM haina mashaka wala wasiwasi na Dkt .Samia kwakuwa inauhakika na uwezo wake na hata utendaji wake kwani wamemuona katika kipindi chake cha miaka minne alichokaa madarakani. Jumaa amesema hayo Oktoba 15 ,2025  wakati akizungumza na Wananchi wa Kata ya Kwala ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa mikutano yake ya kampeni kwa ajili ya kuomba kura ili ifikapo Oktoba 29 waweze kumchagua kuwa mbunge,kumchagua Rais Samia pamoja na diwani wa Kata hiyo Mansour Kisebengo. Amesema Dkt.Samia wakati anaingia madarakani wengi walisema hatoweza...

SHILINGI TRILION 2.34 KUKUZA SEKTA YA KILIMO

Image
  Timothy Marko DmNewsonline .               DAR ES SALAAM. KATIKA kuhakikisha Sekta ya Kilimo inaimarika, Taasisi ya Trust Pass imewezesha kutoa  mikopo  ya zaidi ya  Shilingi Trilioni 2.34 kwa ajili kukuza Sekta hiyo inayochangia Asilimia 60 ya Pato la Taifa Nchini. Akizungumza katika kongamano la  Wafanyabiasha lililofanyika Jijini Dar es Salaam  Octoba 13,2025 na Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Sixtus Mapunda amesema kuwa zaidi ya Asilimia 60 ya Ajira kwa Wananchi imekuwa kichagizwa na Sekta ya Kilimo. "Lazima Kama Watanzania tuifungamanishe Mifumo ya Elimu nakilimo ilikuweza kukuza Soko la Ajira Nchini"Amesema Mkuu wa  Wilaya Temeke Sixtus Mapunda. Mapunda Ameongeza kuwa Nchini Nyingi Duniani zinategemea Rasmali za kukuza Uchumi kutokana Sekta ya Kilimo. Amesisitiza kuwa Takriban Shilingi milioni 2.8 ya Mikopo ya Trust Pass imewekeza katika Sekta hiyo. "Nivyema mifumo ya kifedha ikiaungamanisha na Vyama vya Ushiri...

KATIBU MKUU AMWAGA PONGEZI KWA UWT TABORA

Image
   Na Allan Kitwe, DmNewsonline                  Tabora JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoani Tabora imepongezwa kwa kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwao katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani. Pongezi hizo zimetolewa jana na Katibu Mkuu wa UWT Taifa Suzane Kunambi alipokuwa akiongea na mamia ya Viongozi na wanachama wa Jumuiya hiyo kutoka Wilaya zote 7 za Mkoa huo na vikundi vya wanawake wajasiriamali. Ameeleza kuwa umoja na mshikamano unaoendelea kuoneshwa na akinamama wa UWT Mkoani hapa na wanaCCM wote ni ishara tosha kuwa wagombea wote wa CCM watapata ushindi wa kishindo. ‘Wanawake wa Tabora hongereni, kazi yenu ni njema sana, naamini Oktoba 29 mwaka huu, mtajitokeza kwa wingi zaidi na kumpigia kura za kishindo mgombea Urais kupitia CCM, wabunge na madiwani, CCM Oyeee’, amesema. Kunambi amesisitiza kuwa ni wajibu wa wana UWT kushiriki kikamilifu katika kampeni zinaz...