Posts

Showing posts from October, 2025

*“UCHAGUZI MKUU WA 2025 NI HALALI” – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI*

Image
Na Mwandishi wetu ,DmNewsonline MWANASHERIA  Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025 unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba, 2025 ni halali kwakuwa umefuata misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria za Uchaguzi. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameyasema hayo katika Mkutano na Vyombo vya Habari uliofanyika Ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma, tarehe 28 Oktoba, 2025. Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Johari amesema kuwa Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kuwa, ni haki ya kila Mtanzania aliyetimiza umri wa miaka 18 kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani kama ilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  “Ibara ya 5(1) ya Katiba yetu inatoa haki kwa kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane kupiga kura katika ucha...

MASANINGA : DKT. SAMIA AMEFANYA KAMPENI ZA KIUNGWANA MATARAJIO YA USHINDI NI MAKUBWA.

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                      MKURANGA  MGOMBEA udiwani wa kata ya kiparang,anda wilaya ya mkuranga  Mariam Masaninga ametumia siku ya leo kutoa pongezi zake za dhati kwa mgombea nafasi ya  Rais Dkt. Samia  Suluhu Hassan kwa kufanikisha kumaliza kampeni zake kwa amani na utulivu mkubwa  Masaninga amesema kuwa Mgombea huyo wa Urais ameweza kuzunguka Nchi nzima kwa kufanya kampeni zake na hatimaye leo kufikia tamati. Masaninga ameyasema hayo leo Oktoba 28 2025.Wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za CCM kata ya kiparang,anda ambapo amesema kuwa mbali na kumpongeza Mgombea urais wa CCM lakini pia anamshukuru Mungu kwa kumaliza salama kampeni zake. Amesema kuwa ili kuwa ni miezi miwili ya mchakamchaka  hekaheka lakini leo tunamshukuru Mungu kwa kufikia tamati leo na matarajio ni makubwa mno kupata ushindi  wa kishindo kabisa  Pia Masaninga amesema kuwa...

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline              DAR ES SALAAM VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja na uzalendo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, wakisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa ustawi wa taifa na ibada halisi kwa Mungu. Wakizungumza leo Oktoba 27, 2025, katika Kongamano la Amani la Kitaifa kuelekea Uchaguzi Mkuu, lililofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, viongozi hao wamesema jukumu la kulinda amani ni la kila Mtanzania, bila kujali dini wala itikadi. Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dkt. Abubakar Zuberi, amesema viongozi wa dini wana wajibu wa kuhakikisha jamii inaendelea kuwa na amani, upendo na uzalendo, hasa katika kipindi nyeti cha uchaguzi. “Sisi kama viongozi wa dini tunalazimika kufanya kazi waliyofanya mitume kuhakikisha amani inakuwepo ulimwenguni. Ukiwa na uzalendo utatunza amani, na kutunza amani ndiyo dini,” amesema ...

MJUMBE WA KAMATI YA SIASA MKOA WA PWANI DKT. TINDWA ATOA UJUMBE NZITO UFUNGAJI KAMPENI KISARAWE

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline             KISARAWE  MJUMBE wakamati ya Siasa Mkoa Pwani Dkt  Chakou Tindwa Amewaeleza watanzania na wananchi wa kata ya Makurunge wilaya ya kisarawe kwamba waendelee kukuamini Chama Cha Mapinduzi CCM kwani kinafanya kazi kubwa ya kuwaletea Maendeleo. Dkt Tindwa ameyasema hayo leo Octoba 26, 2025 wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi ngazi ya Ubunge Jimbo la kisarawe ambapo amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi ukiangalia katika upande wa miundombinu ya Barabara ,afya ,umeme, shule ,maji utaona kwamba Kuna kazi kubwa imefanyika . Amesema ifike wakati kuachana na porojo ambazo zinasemwa na watu wasiolitakia mema Taifa badala yake wapime wenyewe kazi hizo ambazo zinafanywa na viongozi thabiti wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi CCM. Amesema mambo yanayofanyika katika maeneo hayo ambayo ameyataka utagundua kuwa Tanzania IPO juu ya majirani wanaoizunguka nchi na unaweza kuthibitisha hayo kwa kuangalia takwimu na si mane...

ASAS : WANANCHI JITOKEZENI KUPIGA KURA MSIWE NA HOFU .

Image
Na Eliasa  Ally,DmNewsonline                 IRINGA  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas amewataka wananchi katika Halmashauri ya Mji Mafinga kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu na kuwaondoa hofu ya kuwa siku hiyo kunaweza kuwa na vitendo vya vurugu kama ambavyo imekuwa ikienezwa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya watu wenye nia ovu. Katika siku za hivi karibuni kumezuka wimbi la baadhi ya watu kutoka ndani na nje ya nchi ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiyashawishi makundi mbalimbali katika  jamii likiwemo kundi la vijana kufanya maandamano na kuchochea ghasia ambazo zitaathiri zoezi hilo la Uchaguzi na amani kwa ujumla wapuuzwe. Asas ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amesema hayo wakati akihutubia maelfu ya wana CCM na wananchi kwa ujumla waliofurika kwenye Mkutano Mkubwa wa Kufunga Kampeni za Chama hicho kwa Jimbo la Mafinga Mjini uliofanyika kati...

MASANINGA, AHITIMISHA KAMPENI ZAKE KIJIJI ALICHOZALIWA MAGOZA MKURANGA

Image
 Na Mwandishi wetu, DmNewsonline              MAGOZA _MKURANGA MGOMBEA Udiwani kata ya kiparang'anda wilaya ya  mkuranga mkoani Pwani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM  Mariam Masaninga amewaomba wananchi wa Kijiji Cha magoza kuwa ifikapo Octoba 29, mwaka huu waenda kukipigia kura Chama hicho ili kiendelee kuwaletea Maendeleo . Amewaeleza wananchi hao kuwa yeye kama mzaliwa wa Kijiji Cha magoza kata hiyo ya kiparang'anda anawaomba kwa moyo wa huruma kwenda kumpa kura Dkt .Samia Suluhu Hassan ,Mbunge wa Jimbo hilo   Alhaj ,Abdallah Ulega na yeye Mariama Masaninga kwa nafasi ya  diwani . Masaninga ameyasema hayo leo Octoba  25, ,2025 alipokuwa anahitimisha kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi wa Kijiji Cha magoza  katika nafasi ya Udiwani ili wamchague awe kiongozi wao kwa miaka mitano ijayo . Mariam  amewaeleza wananchi hao dhamira ya dhati ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya kuendelea kuwatumikia watanzania na...