OFISI MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUFANYA MREJESHO WA GHARAMA ZA UCHAGUZI .

 Timothy Marko DmNewsOnline 

          DAR ES SALAAM. 

OFISI ya msajili wa vyama vya Siasa Nchini  imevitaka Vyama vya Siasa Vilivyo Shiriki Uchaguzi Mkuu October 29,2025 kufanya Mrejesho wa taarifa za Gharama za  Uchaguzi. 

Akizungumza Leo Machi 10,2026 Naibu  Msajili wa vyama vya Siasa Nchini Mohamed Ahmed amesema lengo la kuwakutanisha  vyama hivyo nikuweza kutoa Elimu juu ya sheria za Gharama za Uchaguzi .

"Tuliwapa vyama vya Siasa siku 112 kuweza kurejesha fomu za Gharama za Uchaguzi"Amesema Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa
Ahmed Mohamed.

Naye,Katibu Mkuu wa Chama Cha NLD Doyo Hassan Doyo amesema kuwa Warsha hiyo itawasaidia vyama vya Siasa  kujua Sheria za Gharama za Uchaguzi. 

Aidha,Naibu Katibu Mkuu wa chama cha Umma Bara Simbo Benson amesema Sheria hiyo itawezesha kufahamu mstakabali wa wagombea hao katika uchaguzi Ujao 2030.

Naye Katibu Mkuu wa Chama Cha ACT Wazalendo Ester Thomas amesema  lengo la warsha hiyo ni kutoa Elimu kwa Wagombea juu ya Gharama za Uchaguzi na mchakato mzima wa upatikanaji wa fedha hizo wamezipata wapi  Chama kisichotekeleza hayo kitaweza kupata adhabu kwa mujibu wa sheria. 

Pia amesema lengo ni kujua fedha hizo umezipata wapi zinatoka wapi na taasisi ipi kwasababu kumekuwa na taasisi za kutoka nje zenye nia ovu.   


Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.