VIONGOZI WA NCHI MBALIMBALI WAKUTANA KUJADILI MASUALA YA UHARAMIA WA MAJINI


Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM 

WAZIRI wa Uchukuzi Prof.Makame Mbawara amekutana na viongozi kutoka nchi mbalimbali 
kujadili changamoto za  uharamia wa majini  unaofanyika kwenye Bahari ya Hindi.

Akizungumza  na waandishi wa habari Novemba 28,2024 Jijini Dar es salaam  Waziri wa Uchukuzi Prof.  Mbarawa amesema kuwa mwaka 2007 walikutana na wadau hao ili kujadili uharamia unaofanyika na kuweka mpango mkakati na  kanuni zinazohusu usafiri wa majini .

"Mwaka 2018 tulitayarisha mipango na kanuni maalumu za kulinda sekta za usafiri majini ambazo zilitengeneza uangalizi  wa kupambana na uharamia kwenye bahari.

 Ameongeza  kuwa kipindi cha nyuma tulikuwa na waharamia wa kupanda kwenye meli hivyo kwa sasa tunaangalia uharamia wa vitu mbalimbali vikiwemo uharamia wa madawa na uvuvi haramu.

"Mwaka 2023  kulikuwa na watu ambao wanaingia kwenye meli na kufanya Mauaji hivyo hupekelea meli kuzunguka mbali na kusababisha ongezeko la mafuta mengi" amesema Waziri Prof.Mbawara

Waziri wa Uchukuzi PRof.Mbawara ameeleza kwamba maeneo mbalimbali tumeweka mkakati wa kupambana na maharamia hao ili bahari zetu ziwe salama kwani zikiwa salama biashara zinakuwa nzuri na wananchi wanapata bidhaa kwa bei nafuu na kwa urahisi.

"Uharamia ukikithiri kwa wingi meli haziwezi kuingia nchini kwa wakati hivyo na kuleta usumbufu kwa watumiaji na hatimaye  bidhaa kuwa juu na adimu",amesema Prof.Mbawara.


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa IMO ,Arsenio Dominguez ameongeza kuwa tunaongeza  ulinzi na usalama kwenye meli zote baharini ili kuimarisha shughuli zote  zinazofanyika baharini ,hata hivyo tunashukuru kwa kuweza kushiriki mkutano wa Saba  wa Juuu wa Utekelezaji wa kujadili na  kutatua changamoto zinazojitokeza kwenye vyombo vya majini.




Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025