CCM YASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA NA VITONGOJI




Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline

Chama cha Mapinduzi CCM kimeshinda nafasi 12,150 (99.01%) kwenye nafasi ya Wenyeviti wa Vijiji katika Vijiji vyote 12271 vilivyofanya Uchaguzi huku CHADEMA ikishinda nafasi 97 (0.79%).

Akitangaza matokeo ya jumla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usiku huu, Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa amesema ACT Wazalendo imeshinda nafasi 11 (0.09%) , CUF imeshinda nafasi 10, NCCR , UMD na ADC wameshinda nafasi moja kila Chama.

“Vijiji tisa havijafanya Uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo vya Wagombea baada ya uteuzi” — Mchengerwa.

Chama cha Mapinduzi 'CCM' Pia kimeshinda nafasi 62728 sawa na asilimia 98.26 kwenye nafasi ya Wenyeviti wa Vitongoji Nchini ikifuatiwa na CHADEMA ambayo imeshinda nafasi 853 (1.34%) katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika jana.

ACT Wazalendo imeshinda nafasi 150 (0.23%) , CUF imeshinda nafasi 78, NCCR nafasi 10, UDP nafasi 6, UMD nafasi mbili na ADC wameshinda nafasi moja.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025