CCM YAAHIDI KUWATUMIKIA WANANCHI PASIPO KUCHOKA



Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM 


KATIBU wa NEC Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Taifa CPA Amos Makala amesema kutokana na ushindi tutaenda kuwatumikia wananchi pasipo kuchoka kwani ushindi wa Chama unatokana na kuaminiwa na wananchi.


Akizungumza na wanahabari Novemba 29,20240 katika Ofisi ndogo za CCM Lumumba  Jijini Dar es Salaam, CPA. Makalla amesema, ushindi wa vyama vyote unatokana na wingi wa kura za wananchi.

Aidha amesema uhalali wa ushindi wao  umetokana na wananchi kwa kazi nzuri ambayo chama hicho imekuwa ikifanya hususani katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na utatuzi wa kero kwa wananchi wake.

" CCM inatambua kuwepo kwa changamoto katika uchaguzi huu uliopota wa Serikali za Mitaa, hivyo amewasisitiza viongozi wa vyama vyote vya siasa kushirikiana ili waweze kutatua changamoto hizi zisijirudie katika chaguzi zijazo",amesema CPA Makala.

CPA Makala amesema kwamba tunatambua kwamba zipo changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika uchaguzi huu lakini tushirikiane vyama vya siasa ambao ni wadau 
kuhakikisha na sisi tunakuwa sehemu ya kutatua changamoto hizo hususani katika wakati wa uteuzi wa wagombea.

Alieleza kuwa tujitahidi kutoa elimu kwa wagombea wetu hususani katika ujazaji wa fomu kila mmoja kujaza fomu kwa umakini na usahihi na kufanya hivyo kutaondoa sintofahamu kwa wahusika

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025