GODFREY MZAVA : RAIS SAMIA AMEWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA WAWEKEZAJI NCHINI.




Na mwandishi wetu,DmNewsOnline
 IRINGA 

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Godfrey Mzava amesema  Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wake Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ili waweze kuweleza. 

Mzava ameyasema hayo Leo Juni 25, 2024  mkoani Iringa wakati akizindua kituo cha Mafuta cha Asas kilichopo eneo la kituo kikuu cha mabasi mkoani humo wenye thamani ya Bilioni 1.

 Mzava dhamira ya Rais Samia ni kuhakikisha anasogeza karibu sekta binafsi ili ziweze kufanya kazi na kuleta tija kwa Taifa.

Amesema ili kufikia adhma hiyo Mhe. Rais amezielekeza  taasisi zote za kibiashara na uwekezaji  kuhakikisha  zinaandaa mazingira rafiki, wezeshi na rafiki pasipokuwa na rasimu ili kuwavutia wawelezaji.

"Ninapongeza kampuni ya Asas kwa kuweleza kituo cha Mafuta kama walivyosema kwenye risala yao kuwa kitaendelea kutoa huduma kwa wananchi hasa watumiaji wa kituo  kikuu cha mabasi cha mkoa wa Iringa lakini pia kitaongeza mapato ya Halmashauri.



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025