Klabu ya Yanga imetangaza rasmi kumsajali kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia Clatous Chota Chama ambaye ameondoka Simba SC baada ya mkataba wake kumalizika.
Na Mwandishi Wetu DAR ES SALAAM UONGOZI wa Shirikisho la Vyama vya Waganga wa Tiba Asili Tanzania (Shivyatiata) uliokasimishwa madaraka ya muda wa mwaka mmoja kuliongoza hadi likae sawa, unalalamikiwa na wachama wa vyama vya waganga wa tiba asili nchini kwa kuhodhi madaraka kwa miaka nane kinyume cha sheria na utaratibu waliokubaliana. Wakizungumza na Mwandishi wa DMNews online Tanzania Disemba 31, 2025 baadhi ya wanachama wa vyama vya waganga wa tiba asili kutoka vyama 28 vinavyounda shirikisho hilo, kwamba uongozi uliopo si halali wakidai haukuchaguliwa kikatiba. Pia, wamesema kuwa uongozi huo wa Shirikisho umeshindwa kutimiza majukumu na malengo ya Serikali kuukasimisha madaraka ya muda badala yake unalitumia kujinufaisha wenyewe ikiwamo kufifisha shirikisho kwa kulikosesha dira. Mwenyekiti wa Umoja wa Watengeneza Bidhaa Asili Tanzania (UWABIATA) Rajab Ha...
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline Berlin Ujerumani NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Watu wenye Ulemavu unaofanyika jijini Berlin, Ujerumani tarehe 2 hadi 3 April,2025. Mkutano huo umeandaliwa na Shirikisho la Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu (IDA), Serikali ya Ujerumani, na Serikali ya Jordan na kufunguliwa rasmi kwa pamoja na Kansela wa Ujerumani Mhe. Olaf Scholz na Mfalme Abdullah II wa Jordani. Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano huo Mhe. Scholz amesisitiza juu ya umuhimu wa kushirikiana kimataifa kukuza haki na ujumuishaji wa masuala ya Watu Wenye Ulemavu. “Ushirikiano wa kimataifa ni nguzo muhimu katika kuhakikisha haki na ujumuishaji wa watu wenye ulemavu unatekelezwa kikamilifu duniani kote kwa kushirikiana, serikali, mashirika ya kimataifa, sekta binafsi, taasisi za elimu...
Comments
Post a Comment