Na Mwandishi Wetu DAR ES SALAAM UONGOZI wa Shirikisho la Vyama vya Waganga wa Tiba Asili Tanzania (Shivyatiata) uliokasimishwa madaraka ya muda wa mwaka mmoja kuliongoza hadi likae sawa, unalalamikiwa na wachama wa vyama vya waganga wa tiba asili nchini kwa kuhodhi madaraka kwa miaka nane kinyume cha sheria na utaratibu waliokubaliana. Wakizungumza na Mwandishi wa DMNews online Tanzania Disemba 31, 2025 baadhi ya wanachama wa vyama vya waganga wa tiba asili kutoka vyama 28 vinavyounda shirikisho hilo, kwamba uongozi uliopo si halali wakidai haukuchaguliwa kikatiba. Pia, wamesema kuwa uongozi huo wa Shirikisho umeshindwa kutimiza majukumu na malengo ya Serikali kuukasimisha madaraka ya muda badala yake unalitumia kujinufaisha wenyewe ikiwamo kufifisha shirikisho kwa kulikosesha dira. Mwenyekiti wa Umoja wa Watengeneza Bidhaa Asili Tanzania (UWABIATA) Rajab Ha...
Na Angelina Mganga -DmNewsOnline BDAR ES SALAAM UCHAGUZI wa nafasi ya Uwenyekiti na Katibu Mkuu wa Umoja wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam umefanyika Leo Juni 20,2026,na umemalizika kwa amani na utulivu. Uchaguzi huo ulikuwa na wagombea watatu ambao wamewania nafasi hiyo ya Uwenyeviti wa Wenyeviti wa Serikali ya Mtaa Mkoa wa Dar es Salaam Wagombe wa nafasi ya Uwenyeviti ni Consolatha M.Rwiza Juma A.Mwingano na Razalous A.Mwakiposa Katika uchaguzi huo Razalous A.Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi hiyo ya Uwenyekiti huku Peppino Sudi Peppino akishinda nafasi ya Katibu. Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo,Msimamizi wa Uchaguzi Kambi Sinde amesema kuwa kura zilizopigwa ni 37 na wagombea walikuwa Consolatha M.Rwiza (11),Juma A.Mwingano (2 )na Razalous A.Mwakiposa ( 24 ) hakuna kura iliyoharibika. Razalous A.Mwakiposa ameshinda Kwa kura 24 kati ya kura 37zilizopig...
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, Dkt. Michael Chabai. Na Yusuph Mussa,DmNewsonline KILINDI MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, Dkt. Michael Chabai amesema barabara za wilaya hiyo bado ni changamoto, na kueleza moja ya sababu ya wakulima kuuza mazao yao kwa bei ya chini ni kutokana na changamoto ya barabara hizo. Ameyasema hayo Agosti 22, 2026 wakati anafungua kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, na kuongeza kuwa jitihada zinahitajika kwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha wanafanyia matengenezo ya mara kwa mara barabara za vijijini ili kuona wakulima wanakuwa na uwezo wa kwenda kuuza mazao yao sokoni. "Barabara zetu kwenye wilaya yetu bado ni changamoto, na hii inasababisha mazao ya wakukima wetu kuuzwa kwa bei ya chini. Hivyo tunataka kuona barabara hizo zinapitika ili wakulima wetu waweze kufikisha mazao yao sokoni" alisema Dkt. Chab...
Comments
Post a Comment