Posts

HIFADHI YA TAIFA RUAHA YAWAITA WANANCHI KUSHEREHEKEA MIAKA 60 YA KUAZISHWA KWAKE.

Image
Na Eliasa Ally ,DmNewsOnline   IRINGA   MKUU  wa Hifadhi ya Ruaha Mkoa wa lringa, Godwel Ole Meing’ataki Amewataka Wananchi kwenda kutembelea hifadhi ya Taifa  Ruaha kama Moja ya Kuunga mkono sherehe za maadhimisho ya miaka 60 tangu uwepo wa Hifadhi hiyo.   Akizungumza  na wandshi wa Habari mwishoni mwa wiki  katika maandalizi ya  kulekea  maadhimisho hayo ya  mika 60 ya hifadhi hiyo . Amesema kuwa sherehe za maadhimisho hayo  zitatanguliwa  na shughuli mbali mbali za kijamii pamoja na elimu juu ya umuhimu wa Hifadhi. Ameongeza  kuwa Hifadhi imejipanga kuimarisha uhusiano na jamii mbalimbali, ikiwemo watu wenye ulemavu, kwa lengo la kuwapatia fursa ya kutembelea hifadhi hiyo pamoja na kutoa msaada kwa familia zenye mazingira magumu “Nitumie fursa hii kuwakaribisha Watanzania wote, hususani wakazi wa Iringa, katika maadhimisho ya miaka 60 ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambayo yatafanyika kuanzia octoba 1 hadi 7 2024, amb...

MBUGE SHABANI SHEKIRINDI AWAONYA WANAOCHONGANISHA WANANCHI NA SERIKALI

Image
Na Ashrack Miraji,DmNewsOnline    TANGA  MBUNGE wa Jimbo la Lushoto mkoani Tanga, Shabani Shekilindi ametoa onyo kwa watu ambao wanachonganisha wananchi na Serikali. Shekilindi ametoa kauli hiyo wakati akiwa kwenye mahafali ya wahitimu wa darasa la saba ambao katika Shule ya Msingi Mkurumuzi iliyopo kijiji cha Bombo kata ya Makanya wilayani humo. "Ndugu zangu mimi sitokubali kwa kikundi cha watu wachache ambao wana uchu wa madaraka kuja kuwarubuni wananchi wa kata hii kwa sababu ya maendeleo ambayo yanatekelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni makubwa na ni lazima tudumishe upendo," amesema. "Tusiwe wachoyo wa fadhila kwa kumshukuru Rais Samia kwa kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo la Lushoto hasa kata ya Makanya,  kata hii imepokea zaidi ya Sh.billion moja kwenye sekta ya elimu kwa kujengewa Shule ya Sekondari  Bombo A, na sasa tunaanza kujenga mabweni ya kisasa kwa ajili ya watoto wetu ambao walikuwa wanapata changamoto ya elimu kwa kutembea umbali mrefu kwend...

RAIS SAMIA ATIMBA MSIKITI WA TUNDURU

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline RUVUMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishukuru mara baada ya kusomewa  Dua katika Msikiti Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mkoani Ruvuma leo tarehe 27 Septemba, 2024.

RAIS SAMIA AZINDUA SEKONDARY YA WASICHANA NAMTUMBO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline RUVUMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mchepuo wa Sayansi na Sanaa Namtumbo Mkoani Ruvuma iliyopewa jina la ya Dr.Samia Suluhu Hassan ambayo ujenzi wake umegharimu Shilingi Bilioni 4.6 leo September 27,2024.

ZIFAHAMU SERA ZA CHAMA CHA NATIONAL LEAGUE FOR DEMOCRATY(NLD)

Image
 Na mwandishi wetu ,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  CHAMA  cha NLD kimejikita katika sera za Uzalendo, Haki, na Maendeleo kwa lengo la kuleta mabadiliko nchini Tanzania. Tafsiri Sahihi ya Uzalendo, Haki na Maendeleo *Uzalendo:* unahusisha kujitolea kwa taifa, kuheshimu tamaduni na mila za nchi, na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata fursa sawa. *Haki:* inajumuisha kulinda haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, na kutoa nafasi kwa raia kushiriki katika maamuzi yanayohusu nchi yao. *Maendeleo:* ni kuhusu kuboresha maisha ya wananchi kupitia elimu, afya, na uchumi endelevu. NLD inasisitiza kuwa maendeleo yanapaswa kuwa jumuishi na yanayohakikisha usawa kati ya makundi yote katika jamii. Kwa hiyo, sera hizi zinaungana kuunda mazingira bora ya kisiasa na kiuchumi kwa wananchi wa Tanzania pindi wakikipa ridhaa Chama cha NLD.

BENKI YA NMB KUENDELEA KUSAIDIA JAMII.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  PWANI  BENKI ya NMB imetoa misaada ya Afya na Elimu kwa Zahanati tatu na Shule za Msingi mbili na Sekondari moja kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani vyenye thamani ya shilingi milioni 21. Pia wametoa  madawati 100 na viti na meza 50 kwa Shule hizo, vitanda sita, viti vya kusubiria wagonjwa sita, vipimo sita vya kupimia shinikizo la damu na magodoro sita. Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson John akipokea vifaa hivyo kwenye Shule ya Sekondari ya Dkt Samia Suluhu Hassan mapema wiki hii  amesema kuwa benki hiyo imefanya jambo zuri kuisaidia serikali kupitia sekta ya afya na elimu. John amesema kuwa miradi hiyo ni muhimu sana kwani wananchi bila ya kuwa na afya njema hawawezi kufanya shughuli zao. Naye meneja wa Kanda Seka Urio amesema kuwa benki imekuwa ikitoa misaada kwenye sekta ya afya na elimu na kwa wananchi wanaokumbwa na majanga. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Regina Bieda amesema kuwa benk...

KISHINDO CHA RAIS SAMIA MKOANI RUVUMA NI BALAA.. MAELFU WAJITOKEZA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline RUVUMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Maelfu ya Wananchi wa Kata ya Litola Wilaya ya Namtumbo waliofurika Barabarani kumlaki wakati wa Ziara yake Mkoani Ruvuma leo leo September 26, 2024.