Posts

CCM KIBAHA MJI YATOA TAMKO LA KULAANI VITENDO VYA MAUAJI YA BODA NA ALBINO

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline KIBAHA  CHAMA cha mapinduzi Wilaya ya Kibaha mjini (CCM) kimelaani vikali vitendo vya  matukio ya mauaji ya madereva wa boda boda yanayoendelea katika maeneo  mbali mbali. Akitoa tamko hilo katika kikao cha halmashauri kuu ya chama Mwenyekiti wa (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka alisema kwamba wameamua kwa pamoja kutoa tamko hilo kutoka na kukithiri kwa matukio hayo. Nyamka amesema kwamba matukio hayo ya unyang'anyi wa kuporwa pikipiki na kufanya mauaji yanafanywa na kikundi cha majambazi. Amefafanua kuwa hivi karibuni kumetokea tukionla Katibu wa CCM tawi la Miswe kata ya Mbawa ambapo ndugu Sitaki Pazi kuporwa pikipiki na kuuwawa. Pia Mwenyekiti Nyamka amesema kwamba chama pia kinalaani vikali mauaji ya kikatili aliyofanyiwa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (Albino)  Asimwe Novat mwenye umri wa miaka miwili na nusu. Katika hatua nyingine chama cha mapinduzi kimetoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa hatua ambazo limeanza kuzichukua na kuwatia mba...

TASAC YATOA ELIMU KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

Image
Na Mwandishi Wetu.DmNewsOnline  DODOMA SHIRIKA  la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limewaagiza watoa huduma za usafirishaji majini ikiwemo mawakala wa uondoshwaji na uondoaji mizigo bandarini, kuhakikikisha wanafuata sheria na taratibu za usafirishaji mizigo ili kuondoka usumbufu. Hayo yamesemwa leo Juni ,23,2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC)  Mohamed Salum wakati akizungumzia majukumu ya TASAC katika utoaji huduma na bidhaa kwa watoa huduma bandarini na bandari kavu kwenye maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ya katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. Salum amesema watoa huduma na bidhaa ni vizuri wafuate viwango vinavyotakiwa, ili wateja waweze kuhudumiwa kwa wakati na uhakikikisha wasafirishaji wanapata huduma kwa wakati na kuondoka usumbufu. "Changamoto kubwa wanazopitia ni kwa wateja kutofahamu haki zao hivyo TASAC hivi sasa inasajili wateja ili kubaini mizigo yao inapopotea na kuifuatilia...

KATIBU MKUU CCM AKUTANA NA KOMRED TANG DENGIIE KUTOKA CHAMA CHA CPC, DAR ES SALAAM

Image
Na MwandishiWetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM                   KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt Emmanuel John Nchimbi akiwa kwenye mazungumzo na Komredi Tang Dengjie, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), yaliyofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, jijini Dar Es Salaam, mwishoni mwa juma lililopita. Komredi Dengjie na ujumbe wake, amefanya ziara ya kikazi ya siku 3 nchini.

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA KUPIGA VITA DAWA ZA KULEVYA KANDA YA KASKAZINI YAADHIMISHWA LEO

Image
Na Ahmed Mahmoud,DmNewsOnline   KILIMANJARO  SERIKALI imesisitiza kuweka nguvu zaidi kwa wote walioathirika na urahibu wa dawa za kulevya kwa kuwapatia huduma stahiki ikiwemo kuwarudisha katika maisha ya kawaida na kuwapatia Elimu ya ujasiriamali sanjari na mikopo.   kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya kimataifa kupinga dawa za kulevya nchini inaakisi malengo ya mapambano ya vita dhidi ya dawa za kulevya ili kuikinga Jamii hususani Watoto na vijana wasijihusishe na matumizi Wala biashara haramu dawa. Hayo yamesemwa na  Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Charles Mkombachepa akimuawakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga dawa za kulevya Duniani  kwa Kanda ya kaskazini . Maadhimisho hayo yamefanyika jijini  Arusha kwa ushirikiano na Kanisa la wasabato na DCEA Kanda ya kaskazini yenye kauli mbiu; "wekeza kwenye Kinga na tiba dhidi ya dawa za kulevya". Mkombachepa amesema kauli hiyo inatoa ujumbe ...

MWALIMU COMMERCIAL BANK PLC YATANGAZA MKUTANO MKUU WA MWAKA 2024 KUFANYIKA MKOANI IRINGA.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline                  MWALIMU Commercial Bank Plc. (MCB) inafuraha kutangaza mkutano wake mkuu wa mwaka 2024 ambao utafanyika juni , 27,2024 katika Ukumbi wa Masiti, Mkoani Iringa. Mkusanyiko huo wa kila mwaka wa wanahisa ni kipengele cha msingi cha shirika la MCB mfumo wa utawala, kutoa jukwaa la mazungumzo yenye kujenga ushiriki kuhusu mambo muhimu kwa maendeleo na maendeleo ya benki. Mkutano Mkuu ujao wa Mwaka unawakilisha fursa kwa wanahisa  kukagua utendaji wa benki katika mwaka uliopita, kujadili mikakati ya kimkakati, na Kuchangia kuunda mwelekeo wake wa siku zijazo. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, MCB imepata  mafanikio makubwa katika sekta ya benki.Zaidi ya utendaji wa kifedha, Benki ya Mwalimu Commercial inaendelea kujitolea  mipango ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) inayolenga kuinua jamii kote  Tanzania.  Kupitia programu mbalimbali za CSR, benki inaendelea kusaidia elimu,  a...

BANDARI DAR YAPOKEA MELI KUBWA YA MIZIGO

Image
     Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline       BANDARI ya Dar es Salaam imeweka rekodi kwa kupokea meli kubwa ya mizigo yenye urefu wa mita 294.1 tofauti na meli ambazo imewahi kuzipokea hapo awali kwani meli ya mwisho kupokelewa ilikuwa na urefu wa mita 267 hatua inayotafsiriwa kama sehemu ya mafanikio ya uwekezaji mkubwa  uliofanywa katika bandari hiyo.. Akizungumza  na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kwa meli hiyo kwenye  Bandari ya Dar es Salaam  mwishoni mwa wiki hii  Meneja Mizigo Mchanganyiko  wa Bandari ya Dar es Salaam, Abed Gallus amesema kuwa meli ya (MSC ADU -V) imekuwa meli  ya kwanza kubwa  kuwasili katika bandari hiyo kwani ina uwezo wa kubeba makontena 4,000. "Hii ni historia kwetu  kwani hapo awali tulikuwa tunapokea meli zenye urefu wa mita 267  lakini sasa tunauwezo wa kupokea meli zenye uwezo ukubwa wa  mita 305  haya ni mafanikio makubwa kwetu kama Mamlaka ya Usimami...

BALOZI NCHIMBI AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA TIXON NZUNDA SONGWE

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  KILIMANJARO  KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, leo ameongoza maelfu ya waombolezaji wakiwemo viongozi na wananchi kutoka maeneo mnalimbali nchini, walioshiriki mazishi ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, marehemu Tixon Nzunda, yaliyofanyika huko Msinde, Kata ya Mpemba, Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe, Jumamosi Juni 22, 2024. Nzunda, ambaye hadi mauti yanamkuta kwa ajali ya gari Juni 18, 2024, akiwa ziara ya kikazi wilayani Hai, alikuwa mtumishi mwandamizi wa Serikali, akiwa amewahi kutumikia nafasi mbalimbali za utumishi wa umma, ikiwemo kuwa katibu mkuu wa wizara mbalimbali, baada ya kupanda ngazi za utumishi wa umma kutokea kuwa Ofisa wa Serikali ngazi ya wilaya.