TOSCI YAWAASA WAKULIMA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU

    Na Mwandishi wetu,TANGA

TAASISI  ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI ) imeendelea kuwaasa wakulima kujisajili kwenye mfumo wa Ruzuku wa Mbegu.

Kauli hiyo imetolewa leo Octoba ,16,2025 na Mkurugenzi wa Tathimini na majaribio kutoka TOSCI Matenga M. Swai kwenye viwanja vya Usagara Jijini Tanga wakati wa kilele Cha Maadhimisho ya siku ya chakula Duniani yenye kauli mbiu ya Tuungane pamoja kupata chakula Bora kwa Maisha Bora ya Baadae.

Matenga amesema wakulima na Watanzania wote washirikiane kwa pamoja ili wapate Mbegu Bora  na wazingatie Ubora kwa maana hiyo wanunue Mbegu zilizopo kwenye vifungashio na waakikishe wanapewa risti.

Amesema TOSCI imeanzisha mfumo wa usajili Mtandao yaani Online.ambao unasajili kwa mfumo wa Ruzuku kuanzia ngazi ya Wilaya

Ameongeza kuwa  majukumu ya TOSCI ni kushugulikia maswala ya Mbegu kukagua maghala hayo yanafanywa kwa kushirikiana na Maafisa ugani waliopewa mafunzo na TOSCI.

Ameongeza kuwa wanapita kwa wauzaji yaani madukani Lengo ni kuona Mbegu zinanazouzwa zina ubora maana Mbegu ni kitu ambacbo Kiko hai.

 kwa upande wake mnufaika wa mradi wa BBT. Ndogowe(Mama Samia Block farm) DODOMA. NduguHafidhi mambole amesema wamenufaika  vitu vikuu vinne elimu, aridhi,mtaji, pamoja na Masoko

Amesema kupitia TOSCI wamenufaika kwa kupata Mbegu Bora ambazo zinaleta tija kwenye mavuno hali ambayo inapelekea kupata kipato kizuri kinachowasaidia kuendesha uchumi wao   



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.