LUFEZUWA AWATAKA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI

   Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline

          DAR ES SALAAM 

MGOMBEA Ubunge Jimbo la Temeke kupitia chama Cha National Labour Party (TLP),Mohamed Shabani Lufezuwa amewataka watanzania kudumisha amani,kwani amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani

Hayo ameyabainisha na mwandishi katika mahojiano maalum na mwandishi wa Dmnews Jijini Dar es Salaam amesema kwamba "niwaombe watanzania wenzangu siku zimeisha tunakaribia kwenda kupiga kura bado siku chache kwahiyo tukapige kura kwa amani na tukawachague wagombea wa TLP kwa nafasi ya Urais,Ubunge na Udiwani ili tuwaletee maendeleo watanzania

Mgombea Lufezuwa amebainisha vipaumbele kwa maendeleo ya Jimbo la Temeke ambavyo ni elimu,uchumi na huduma za jamii  .

Amesema endapo atapata ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo Hilo nitahakikisha kwamba uchumi unakuwa Kwa Kasi kwa wananchi wa Jimbo la Temeke

"Niwaombe sana ,Watanzania wenzangu,mkapige kura kwa amanu na kukiletea ushindi wa kishindo Chama Cha TLP",amesema Lufezuwa

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.