GEKULA:WANANCHI NICHAGUENI NIWALETEE MAENDELEO MAJOHE.

Mgombea Udiwani kata ya Majohe katikati aliyevaa shaeti la kijani Julius Gekula Warioba akiwasili katika mtaa wa rada Manispaa ya ilala . ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Octoba 29,mwaka huu nchi nzima .

Na Mwandishi wetu,DmNewsonline

                 DAR ES SALAAM

MGOMBEA Udiwani kata ya Majohe Halmashauri ya Ilala jijini Dar es salaam  Julius Gekula Warioba  amewaeleza wananchi wa kata hiyo Umuhimu wa kumchagua kuwa diwani wao na kwamba akiwa katika nafasi za ujumbe wa Serikali ya mtaa na Ofisa mtendaji wa mtaa huko nyuma alifanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

 Amesema anaishukuru Chama chake Cha Mapinduzi CCM na wanaccm wa kata ya majohe kuweza kumwamini na kukubari kupeperusha bendera ya Chama kwa nafasi ya Udiwani hivyo jukumu alililonalo huko mbele baada ya kuchaguliwa Octoba 29,mwaka huu. Nikuwatumikia wananchi hao kwa uweza wake wote.

Gekula ameyasema hayo leo Octoba 16 ,2025 katika mkutano wa kampeni za Chama hicho uliofanyika katika mtaa wa rada  ndani ya kata hiyo ya majohe ambapo amesema wananchi wasifanye makosa na badala yake wajitokeze kwa wingi kukichagua Chama Cha Mapinduzi CCM katika nafasi ya Urais,ubunge na Udiwani.

Akizungumzia mipango na kazi nzuri inayofanywa na Mgombea wa CCM ambaye ndio Rais wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amesema katika Kata ya majohe katika kipindi Cha mwaka  2025 /30 wanatarajia kupata Barabara za lami kuzunguka mitaa mbalimbali na muda wote ujenzi unatarajia kuaza .

Amesema  kata ya majohe serikali chini ya Rais Dkt. samia Suluhu Hassan imejipanga kujenga Barabara  nyingi ili kurahisisha mawasiliano baina ya mitaa na mitaa Lengo likiwa ni kuchochea shughuli za Maendeleo za wananchi wa kata ya majohe na maeneo mengine .

Gekula amesema kuwa zipo Barabara zingine za changarawe ambazo nazo atakwenda kusimamia kuhakikisha zinajengwa na wananchi wanapita bila wasiwasi.

Kuhusu  elimu pia  amesema Mgombea urais wa a CCM Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta fedha  nyingi kujenga madarasa na miundombinu mbalimbali ya shule ili kuwezesha watoto kusoma pasipokuwa na changamoto yeyote.

Gekula amesema kutokana na kazi zote ambazo amezifanya Mgombea huyo wa Urais  amewaeleza wananchi endapo watamchagua eneo hilo la Majohe A  atahakikisha wanajenga zahanati. 

Pia amesema Dkt samia amefanya Maendeleo mengi amejenga vituo vya afya na watajenga zahanati hapo na katika upande wa elimu watajenga shule ya Msingi  na sekondari lakini ujenzi wa vivuko na madara vyote vjtajengwa ili kurahisha wananchi kupita kirahisi.

 "shida ya vivuko kweneye maeneo korofi yote yatashughulikiwa  kikamilifu hivyo wananchi jukumu lenu kubwa ni kuchagua Chama Cha Mapinduzi CCM Octoba 29,mwaka huu."amesema 

Kuhusu Ulinzi na Usalama amesema wamejenga kituo Cha Polisi Majohe juu na jumla ya shilingi  zaidi 113.zitafanya kazi ya kumalizia kituo hicho Cha Polisi hivyo  jukumu lake kubwa nikwenda kusimamia ili kuweza kukamilika kwa kituo hicho.

 Amesema hakuna Maendeleo pasipokuwa na amani hivyo amewaasa wananchi waache mara Moja ndoto ya kutaka kufanya maandamano badala yake wanatakiwa kwenda kupiga kura na kurudi nyumbani. 

" Wanaotaka kuandamana wanatakiwa kuulizwa watoto wao wako wapi na wanasoma wapi na kuirudisha amani mahala ambapo penye machafuko ni kazi kubwa sana "amesema 

katika hatua nyingine amesema akichaguliwa tu anakwenda kusukuma ujenzi wa  ofisi za serikali ya mtaa ili wananchi waweze kupata huduma pasipokuwa na changamoto zozote 

Amewaeleza wananchi kuwa yeye akichaguliwa  huduma zote za serikali ya mtaa ni bure na mwananchi yeyote ambaye atadaiwa fedha basi atoe taarifa kwake. 

Naye Mwenyekiti  CCM kata ya majohe Nuru Mizumo amewataka wanachama wa Chama hicho kuwa wasidanganyike badala yake wampe kura za kutosha Julius Mataro Gekula .

Amesema Mgombea huyo hana shida na na sio kiongozi yule wakujilimbikizia Mali  yeye anajitosheleza  yeye amekuja kusaidia wananchi wa kata hiyo ya majohe .
Amesema jambo kubwa la wanaccm na wananchi kwa ujumla ni kuchagua mafiga matatu ambapo wachague rais anayetokana na Chama Cha Mapinduzi CCM.

Kwaupande wake mgeni mwalikwa Florian Karugaba ambaye alikuwa Mgombea ubunge kivule akizungumza katika mkutano huo wa kampeni uliofanyika katika mtaa wa rada.

Karugaba amesema Rais .Dkt. Samia anatafufa maendeleo na wananchi wasije kudanganyika kwani kiongozi huyo anamalengo makubwa sana kwa Maendeleo ya wananchi wake.

Amesema Dkt. Samia ameleta Urais wa vijana kwenda veta kwani mtoto akimaliza anakwenda veta kupata ujuzi huyo ndio Dkt.samia Suluhu Hassan.    


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.