ULEGA: KATIBA MPYA UHAKIKA KWA DKT SAMIA

 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline

                MKURANGA 

MGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Jimbo la mkuranga Alhaj Abdallah Ulega amewataka watanzania kama wanataka katiba mpya basi wanapaswa kumchagua Dkt Samia Suluhu Hassan kwani yeye alikuwepo katika machakato wa katiba .

Amesema hata katika uzinduzi wa kampeni kitaifa zilizofanyika jijini Dar es salaam Agost 27,2025 katika Viwanja vya Tanganyika perkas amesema ametamka kuwa katika siku 100 za mwanzo atahakikisha anafufua mpya mchakato wa katiba mpya.

Ulega amesema maneno haya leo Septemba 6,2025 katika uzinduzi wa kampeni Jimbo la mkuranga ambapo amesema Dkt .Samia ni muumini wa mariadhiano na akitamka anatenda huyo ndio daktari Samia .

Amesema kuwa jambo Moja tu kwa watanzania na wananchi wa Jimbo la mkuranga ni kuhakikisha wanampigia kura za kutosha mgombea wa Chama Cha Mapinduzi CCM ili aweze kutimiza mambo makubwa  kwa ajili ya maendeleo ya wananchi .

Pia Ulega amezungumzia Barabara ya kilwa  kutoka mbagala rangi tatu hadi kongowe kutanuliwa ili kurahisisha usafiri katika eneo hilo na Juhudi za kufanya kazi hiyo ndio zimeaza.

Waziri ulega akizungumza na wananchi hao wakati akizungumzia Maendeleo na mambo mbalimbali ambayo yamefanyika katika Jimbo la mkuranga amesema wananchi hao wakimpa kura za kutosha na yeye wakimchagua atakwenda kumuomba mama ili kuweza kupandisha hadhi wilaya ya mkuranga na kuwa Halmashauri ya Manispaa ya mkuranga .

Amesema wilaya hiyo inastahili kuwa Manispaa kutokana  na uwepo wa viwanda vya kutosha katika Jimbo hilo ambapo amesema hivi sasa wilaya hiyo inaviwanda vidogo zaidi ya 100 na  viwanda vikubwa zaidi 70 hivyo inastahili mkuranga kuwa Manispaa


Ameongoza kuwa leo umezinduliwa mkutano wa kampeni na  yeye na madiwani wake watafanya  kampeni za Kistarabu na wanakwenda kata kwa kata  ili kumuombea kura Dkt.samia Suluhu Hassan ili kuhakikisha wanapata kura nyingi.

Mgombea huyo pia aliwaeleza wananchi hao kuwa amani ya Taifa ndio inayofanya wajadili viwanda ,na mahala ambapo hakuna amani huwezi Kujadili maji,viwanda ,Barabara,ajira ,na mambo mengine huku akiwaomba viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa .

Amesema kutokana na amani iliyopo leo hii mkristo na muislamu wanaishi nyumba Moja na kupeana hata chakula hilo ni Somo tosha la uwepo wa amani .

Katika uzinduzi wa kampeni hizo pia wananchi kutoka katika vyama vingine vya upinzani ikiwemo wa chama Cha wananchi CUF na wengine kutoka Chama Cha Act _Wazalendo wapato 89 wametangaza kurudi Chama Cha Mapinduzi CCM huku wakiandika ujumbe wa 'TUNARUDI KWA MAMA'   


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025