TLP KUTOA MWAROBAINI WA AJIRA KWA VIJANA

       Timothy Marko,DmNews online 

           DAR ES SALAAM 


WAKATI  kampeni za uchaguzi zikiwa tayari zimeshaaza Kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Octoba 29 mwaka huu Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Tanzania Labor party (TLP)Rwamugira Yustas amesema kama  atachaguliwa kuwa Rais wa Tanzania  atawakopesha Vijana na Wanawake Matrekta madogo madogo ili kuweza kuboresha hali zao kiuchumi kupitia Sekta ya Kilimo.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Rwamugira Yustas amesema kuwa watanzania wakimpa  ridhaa kuwa Rais atahakikisha wakulima Nchini wanapewa pembe jeo zitakazo ratidiwa na wakuu wa Mikoa na Wilaya.

"Hatutaki Mlolongo wa kupata pembejeo , Sambamba na hilo tutaboresha Sekta ya Viwanda Vidogo ili Vijana waweza kupata Ajira."Yustas.

Ameongeza kuwa  ilani ya Chama hicho itawawezesha kupata Mashine za kuunganisha  Vyuma ilikuweza kuchochea Sekta ya Viwanda.

"Nikipewa Ridhaa  na Wananchi Nitahakikisha Vijana wanapatiwa Mikopo na fuu isiyo nariba ili kuweza kuzalisha "Amesisitiza Yustas.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Taifa kupitia Chama hicho, Richard Lyimo amesema yeye kwa wadhifa ni mwenyekiti wa Chama hicho lakini Amepisha Rwamugira Yustas ambaye ni katibu Mkuu wa Chama cha Tanzania Labor party (TLP).

Amesema kuwa hana shaka nauwezo wa Mgombea huyo kwani n mchapa kazi.

"Tumemkabidhi Sera ya Chama ambacho kipaumbele chake ni Kudumisha Amani,Huwezi Kudumisha Uchumi pasipokuwa na taifa lenye Amani"Lyimo.

 Lyimo Ameongeza kuwa katika Kuwania kiti cha Urais atahakikisha Amani inakuwa kipaumbele cha Chama hicho nakusisitiza hawato penda kupata Majeraha Mara baada ya Uchaguzi kukamilika.

"Mgombea Wetu mpeni kura za ndio nitapambana kutatua Changamoto za Usafiri kwa Wanafunzi"Amebainisha Lyimo.

Aidha, Makamu Mwenyekiti Taifa wa Tanzania Labor party (TLP) Johari  Rashid amesema atahakikisha kero ya Upatikanaji wa Bima ya Afya inakwenda kupata majibu

Amesema Kumekuwa na Changamoto za Upatikanaji wa Bima kwa kundi la Wazee na Vijana."Bima ya Afya imekuwa Changamoto sio kwa Wazee bali hata Vijana"Amesema  Johari Rashid .

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025