MSAMA :MAPOKEZI ANAYOPATA MGOMBEA URAIS CCM DKT SAMIA NI ISHARA NZURI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

  Na Mwandishi wetu,DmNewsonline 

        DAR ES SALAAM

MKURUGENZI wa Msama  Promotions, Alex Msama, ametoa pongezi zake kwa Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuonesha ukakamavu wa hali ya juu  tangu alipoaza kampeni Agosti 28,2025.

Msama amesema katika  kampeni alizozifanya kwa wiki kadhaa sasa tena pasipo kupumzika  ni kielelezo kikubwa  cha ukakamavu na dhamira ya kweli ya kuwatumikia Watanzania.

Kauli hiyo ametoa jijini  Dar es Salaam, wakati akizungumza na Waandishi wa habari akizungumzia tathimini yake ya tangu Mgombea huyo Urais kupitia CCM Dkt Samia  Suluhu Hassan aaze ziara zake hizo za kampeni ,ambapo  Msama amebainisha kuwa mapokezi makubwa anayoyapata Dkt. Samia ni dalili tosha za ushindi mkubwa unaomsubiri katika uchaguzi ujao.

Pia amewataka watu wanaoendeleza lugha za matusi mitandaoni kuacha mara moja, nakudai watanzania wasipoteze muda kuwajibu bali wawapuuze kwani wengi wao wanatumiwa na nguvu za kigeni zisizo na nia njema kwa Taifa.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025