WATIA NIA 84 WARUDISHA FOMU ZA UBUNGE WILAYA ILALA

Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline

        DAR ES SALAAM 

WAGOMBEA 84 waliochukua fomu za kutia nia katika nafasi ya  Ubunge  wamerejesha fomu za Ubunge Wilaya ya Ilala katika majimbo  manne ambayo ni Ilala,Segerea,Ukonga na Kivule.

Akizungumza na waandishi wa habari  Leo Julai 2,2025 Jijini Dar es Salaam Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala Chief Sylvester Yaredi amesema mchakato wa kuchukua fomu na kurudisha fomu dirisha limefungwa saa kumi kamili .

Aidha, amesema kwamba  katika zoezi hilo wagombea 87 waliochukua fomu   na Wagombea  84 ndio waliorudisha fomu.

Katibu wa wilaya Yared alisema katika jimbo la Kivule wamechukua fomu 46 wamerejesha 44,Jimbo la Segerea wamechukua 18,wamerejesha 17,Jimbo la ukonga wamechukua 11 na wamerejesha 11,na Jimbo la Ilala wamechukua 12 na wamerejesha 12.   

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025