RC KUNENGE ARIDHISHWA NA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATO HALMASHAURI YA KIBAHA TC

Na Victor Masangu,DmnewsOnline,

                  KIBAHA
 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Alhaji Abubakari Kunenge amempongeza kwa dhati Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha mjini Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuweza kuweka mikakati madhubuti katika  kubuni vyanzo  vipya vya ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo yameweza  kuleta mabadiliko  chanya katika utekelezaji wa miradi mbali mbali ya kimaendeleo.

Kunenge ameyasema hayo wakati wa kikao maalumu cha baraza la madiwani katika Halmashauri ya Kibaha mji kwa ajili ya kuweza kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa kipindi cha kuanzia mwaka  wa 2023  hadi 2024 ambacho kimeweza kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, wakuu wa idara, wataalamu  pamoja na viongozi  mbali mbali  wa chama.

Amesema kwamba Halmashauri ya Kibaha mji imeweza kupiga hatua kubwa hadi kuweza kupandishwa hadhi ya kuwa Manispaa kutokana na juhudi na ushirikiano ambao unafanya na viongozi mbali mbali wakiwemo wakuu wa idara, baraza la madiwani,mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi mtendaji kwa kuweza kushirikiana na viongozi wenzake katika suala zima la kuleta maendeleo katika nyaja mbali mbali.

"Nampongeza sana Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha  mjini Dkt. Rogers Shemwelekwa   pamoja na timu yake nzima  wakiwemo wakuu wa idara, wataaalamu pamoja na baraza la  madiwani ambao kwa kweli mimi siwezi  kuoana sababu ya kutowapongeza  kwa dhati kabisa akiwemo Mbunge pamoja na Mkuu wa Wilaya ambao wameunganisha umoja na ushirikiano katika suala zima la maendeleo bila kusahau juhudi za kupandisha hadhi kuwa  Manispaa,"amebainisha Kunenge.

Aidha Kunenge amewataka viongozi wa Halmashauri ya Kibaha mji kuachana na tabia ya kuwa na mivulugano  na vurugu ambazo hazina tija na badala yake wahakikishe wahakikishe wanaungana kwa pamoja katika kusikiliza na kushughulikia  kero na changamoto  mbali mbali zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha mjini Dkt. Rogers Shemwelekwa  amempongeza Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutenga fedha nyingi ambazo zimeweza kwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo katika sekta ya afya, maji, elimu, miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za msingi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibaha mjini Mussa Ndomba amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na baraza la madiwani kwa kuweza kushirikiana  bega kwa bega katika kipindi chote cha miaka mitano hali ambayo imeweza kuleta mabadiliko  makubwa katika suala zima la kuweza kuongeza kasi kubwa ya maendeleo kwa wananchi.   



                                                   

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025