POLISI DAR WATOA RAI KWA WATUMIAJI VYOMBO VYA MOTO KUFUATA SHERIA

Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa rai kwa watumiaji wote wa barabara kuzingatia Sheria, Kanuni, na matumizi sahihi ya barabara muda wote wanapoendesha vyombo vya moto. Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 31,2025 Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalu ya Dar es Salaam,SACP Muliro Jumanne Muliro amesema mwezi Aprili hadi 31 Mei 2025 jumla ya madereva wa magari na pikipiki za maguruduamu matatu (Bajaj) wamekamatwa kwa kutumia barabara za mwendo kasi kinyume na sheria ni 289, pikipiki(bodaboda) 61, bajaj 65,magari ya Serikali 35, magari binafsi 123,walichukuliwa hatua kali za kisheria na wengine 41walionywa. Aidha ,amesema kwa kutumia kifungu Cha 45 na 46A vya Sheria ya Usalama barabarani sura ya 168 iliyorekebishwa mwaka 2002 kinachokataza dereva kutumia kilevi na kuendesha chombo Cha moto,ufuatiliaji maali usiku na mchana ulifanywa na kuwapima u...