WAZIRI KABUDI KUZINDUA BODI YA ITHIBATI YA WAANDISHI WA HABARI MACHI 3.

Na Mwandishi Wetu, JAB, Dar es Salaam WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Palamagamba Kabudi, Wiki ijayo anatarajiwa kuzindua Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB). Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imeeleza kuwa uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Machi, 03,2025 katika Hotel ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam. Katika Uzinduzi huo Waziri Kabudi pia atamkabidhi zana za Kazi Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Tido Mhando, zinazojumuisha Sera ya Habari, Sheria ya Huduma za Habari na Kanuni zake. Miongoni mwa majukumu ya Bodi hiyo yanayotarajiwa kuanza kutekelezwa mapema mara baada ya kuzinduliwa ni pamoja na kutoa Ithibati na Vitambulisho (Press Card) kwa Waandishi wa Habari waliokidhi vigezo vilivyoainishwa kisheria na kusimamia maadili ya taaluma ya Uandishi wa Habari. Kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imepewa mamlaka...