Posts

Showing posts from August, 2024

ORYX GES YAZIDI KUCHANJA MBUGA YAGAWA MITUNGI NA MAJIKO YAKE 1000 JIJINI MBEYA .

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  MBEYA  SERIKALI imesema kuwa imekuwa na mikakati mbalimbali ya kuhamasisha  matumizi ya Nishati safi ya kupikia nchini na lengo ifikapo 2034 asiliami 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati mbadala ya kupikia. Kauli hiyo imetolewa jijini mbeya Leo Agosti 31 ,2024 na  Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga wakati akikabidhi mitungi na majiko yake 1000 ambayo imetolewa na Kampuni ya Oryx Ges Kwa washiriki wa  mashindano ya kupika kwa gesi ya Oryx jijini humo  Kwa lengo la kuwawezesha kurahisisha shughuli za mapishi. Pia Naibu Waziri  Kapinga amesema  Serikali imewataka wadau wa gesi kuangalia uwezakano wa kuwa na gesi ambayo Mwananchi atanunua kidogo kidogo kila siku ilimkuwezesha wananchi wengi kutumia Nishati hiyo mbadala . Mashindano hayo ya kupika kwa gesi yaliyofanyika kuanzia Agosti 27 na kuhitimishwa leo Agosti 31,2024 yameandaliwa na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt.Tulia Akson kupitia taasisi yake ya Tulia Trust ...

MIAKA 60 YA HIFADHI YA TAIFA MIKUMI YAZAA MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA UTALII

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline  MIKUMI MIAKA  60 ya kuanzishwa kwa Hifadhi ya Taifa Mikumi imekuwa na  mafanikio makubwa katika Sekta ya Utalii nchini yakichangiwa na jitihada zinazofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hayo yamesemwa  leo Agosti 31,2024 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) wakati wa Maadhimisho ya Miaka 60 ya Hifadhi ya Taifa Mikumi iliyoko mkoani Morogoro Waziri Dkt. Chana   amesema kupitia filamu maarufu ya “Tanzania: The Royal Tour” pamoja na filamu ya “The Amazing TANZANIA”zimekuwa chachu ya kukuza utalii na kuongeza idadi ya wageni wa ndani na nje ya nchi. “Kufuatia jitihada hizo za Rais Dkt . Samia, katika mwaka wa fedha 2023/2024 idadi ya watalii wa kimataifa waliofika nchini imeongezeka kwa asilimia 96 kutoka watalii 922,692 Mwaka 2021 hadi kufikia watalii 1,808,205 Mwaka 2023” amesema Nakuongeza "upande wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, kwa mwaka 2023/2024 jumla ya watalii 138,844 wametembelea Hifadhi hiyo ...

CCM KIBAHA MJI YACHUKIZWA NA UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline   KIBAHA CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini kimewataka viongozi wa CCM  kuanzia katika ngazi za Kata, Wilaya na Mkoa kutoingilia kabisa  maamuzi ya wana ccm pamoja na wananchi katika suala zima la  kuwachagua viongozi wanaowapenda katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu kwani wao ndio wanawafahamu  vizuri uwezo wao wa kuchapa  kazi.   Kauli hiyo imetolewa na  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka wakati wa kikao cha Halmashauri kuu  CCM Wilaya ya Kibaha mji ambacho kimefanyika kwa lengo la kuweza  kupitisha utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia Januari  hadi mwezi Juni mwaka 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na chma. Nyamka amebaainisha kwamba lengo  kubwa la chama cha mapinduzi ni kuhakikisha inaweza kushinda kwa kishindo katika mitaa yote hivyo ni wajibu wa viongozi wote wa CC...

RAIS DKT .SAMIA ANATARAJIA KUONGOZA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI BEIJING CHINA.

Image
Na  Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  RAIS wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuongoza  mkutano wa Kilele wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika utakaofanyika kuanzia Septemba 4 hadi  2024 Jijini Beijing, China. Hayo  yamesemwa  Leo Agosti 31,2024 Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo (MB)  amesema kuwa Dkt Samia atashiriki mkutano huo kufuatia mwaliko wa  Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Xi Jinping. " Ushiriki wa Rais Dkt.  Samia kwenye mkutano wa kilele wa FOCAC unalenga kuendeleza  kudumisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na China ambao mwaka huu umetimiza miaka 60 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili",amesema  Aidha kutokana na  makubaliano ya Serikali ya China namna ya kuendelea kuongeza ushirikiano katika maeneo ya kipa...

EMIRATES GROUP CELEBRATES ITS SHINING FEMALE EMIRATI TALENT AND THEIR DEDICATION TO THE GROWTH OF UAES AVIATION INDUSTRY

Image
DmNewsOnline, Dubai The Emirates Group is proud to celebrate the contributions of Emirati women, and the vital work they do to advance excellence across aviation and travel in the United Arab Emirates. The Group has attracted its largest ever pool of Emirati women as new joiners in the last financial year across a range of business functions Emirati women are forging their career paths across a variety of business functions at the Emirates Group and building the foundations for a talent pipeline to support the next generation of aviation professionals.  Approximately 38 per cent of the Group’s Emirati workforce consists of women, and in the last financial year, the organisation welcomed a record number of Emirati women to its workforce.  This further reinforces the Emirates Group’s commitment to integrating Emirati women in the UAE’s growing aviation sector, where they are empowered with the right skills, competencies and expertise, allowing them to thrive and reach their full...

RAIS SAMIA ASHIRIKI MASHINDANO YA KIMATAIFA YA QURAAN, AHIMIZA KUDUMISHA UMOJA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. Tukio hili muhimu limeakisi dhamira ya Rais Samia ya kuendeleza umoja wa kitaifa na kudumisha amani katika nchi yetu. Katika hotuba yake, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa haki, amani, kuheshimiana, na kustahimiliana kama nguzo za kuimarisha umoja wetu kama taifa. Ameeleza kuwa mashindano haya yanachangia katika kuimarisha maadili ya kitaifa na kudumisha mshikamano miongoni mwa wananchi wa Tanzania bila kujali tofauti za kidini au kikabila. Rais Samia pia amegusia umuhimu wa kuendeleza familia zetu na maadili ya nchi, akibainisha kuwa familia yenye misingi imara ni msingi wa taifa lenye nguvu. Amehimiza wazazi na walezi kuhakikisha kuwa watoto wanalelewa katika mazingira ya heshima, amani, na upendo ili kuijenga jamii yenye maadili bora. Aidha, Rais Samia ameweka mkazo juu ya nafasi y...

TAFFA WAMPA ANO RAIS DKT SAMIA KWA MABORESHO YA BANDARI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM CHAMA  cha Wakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) kimepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kuboresha huduma za upakiaji na upakuzi wa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam na kuwataka wanaobeza jitihada hizo kupuuzwa. Akizungumza  katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam   Rais wa Taffa Edward Urio amesema kuwa bandari ya dar es Salaam kupitia uwekezaji uliofanywa na ushirikishwaji wa sekta binafsi imekuwa na mafanikio makubwa ya kujivunia katika kipindi cha serikali ya awamu ya sita. “Tukiwa kama wadau wakubwa wa usafirishaji na upakuaji wa mizigo bandarini, tunajivunia sana uwekezaji mkubwa uliofanyika na kukwazika na watu wanaopinga maendeleo hayo kwa namna moja au nyingine,”amesema Urio. Amesema licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi katika kuhakikisha ufanisi unaongezeka katika utoaji huduma katika bandari ya Dar es...

SERIKALI KUJENGA BARABARA YA MASASI - LIWALE KM 175 KWA AWAMU

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline LIWALE  SERIKALI imesema inaendelea na utaratibu wa ujenzi wa barabara ya Masasi –Nachingwea- Liwale yenye urefu wa KM 175 kwa awamu ili kuendelea kurahisisha shughuli za kiuchumi na biashara kwa wananchi. Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya ameyasema hayo leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Maimuna Ahmad Pathan alietaka kujua ni lini Serikali itaijenga barabara ya Masasi- kwenda Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami. "Spika naomba nimhakikishie Mbunge kwamba taratibu za ujenzi wa barabara hiyo zinafanyika kwa awamu kutokana na upatikanaji wa fedha”, amesema Naibu Waziri Kasekenya. Katika hatua nyingine, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi Milioni 500 kwa ajili ya usanifu na matengenezo ya barabara zilizoathiriwa na mvua katika kipindi cha mwaka 2024 - 2025 ikiwemo barabara ya Kongowe –Mjimwema  Bhadi Kivukoni KM 25.     Naibu waziri Kasekenya alikuwa akijibu swali la Mbu...

DIWANI VISIGA AMUUNGA MKONO RAIS DKT. SAMIA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline KIBAHA    DIWANI wa kata ya Visiga katika Halmashauri ya mji Kibaha Kambi Legeza katika kuunga mkono na  kuchagiza  chachu ya maendeleo katika sekta ya elimu ameamua kutoa msaada wa mtambo  maalumu wa kusaidia  kutolea nakala mbali mbali za karatasi  'Photocopy mashine'  katika shule ya msingi visiga kwa ajili ya kuwasaidia walimu na wanafunzi kuondokana na adha waliyokuwa nayo.  Kambi ametoa msaada wa mashine hiyo wakati  wa sherehe ya  mahafali ya shule ya msingi Visiga ambayo imeandaliwa kwa ajili ya kuweza kuwaaga wanafunzi wanaomaliza  darasa la saba wapatao 248 ambao wamefanikiwa kuhitimu katika hatua hiyo ngazi ya msingi  na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, wakiwemo wa  chama, wazazi , walimu,  walezi pamoja  na wazazi. Kambi amesema  kwamba amesema kwamba ameamua kutoa msaada huo kutokana na  kubaini katika shule hiyo kuna uhitaji mkumbwa kupel...