Posts

BUJURA YAMSINDIKIZA MALONGO KWA SHANGWE KUREJESHA FOMU YA UDIWANI

Image
Na Mwandishi wetu, DmNewsonline                       GEITA  Mgombea udiwani wa Kata ya Bujura kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Malongo Mahamed Salum, leo Agosti 27, 2027, amerejesha fomu ya kugombea udiwani huku akisindikizwa na wananchi wa vijiji vyote vya Ngura kwa bashasha, vifijo, nderemo na shangwe mpaka ofisi za kata. Baada ya kurejesha fomu, Malongo ameahidi kushirikiana kwa karibu na wananchi katika shughuli za maendeleo pamoja na kushirikiana nao katika shida na raha za kila siku. Aidha, aliahidi ushirikiano na viongozi wa ngazi za juu akiwemo Mbunge wa Jimbo hilo ili kupunguza changamoto zinazowakabili wananchi wa Kata ya Bujura. Katika uchaguzi wa kura za maoni, Malongo aliibuka kidedea baada ya kupata kura 434 kati ya kura 513 zilizopigwa, akiwashinda Bundala Charles aliyepata kura 35 na diwani mstaafu Amina Kanijo aliyepata kura 41.   

ÇOMRADE DKT.JOHN NCHIMBI ACHUKUA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA NYASA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                      NYASA          MGOMBEA  wa ubunge Jimbo la nyasa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt.John John Nchimbi amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia chama cha mapinduzi (CCM), kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2025.  Dkt.Nchimbi  amepokea fomu hiyo leo Agosti 26, 2025 , kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la nyasa. Wanaccm na wananyasa kwa ujumla wake walijitokeza kwa wingi katika  hafla hiyo  huku Mgombea huyo mteule akionesha furaha yake na kuzungumza machache  

DKT.JAFARI ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BUSANDA

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                    GEITA  MGOMBEA  ubunge wa kupitia  Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Jimbo la Busanda, Wilaya ya Geita, Dkt. Jafari Rajabu Seif, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa jimbo hilo kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi (INEC). Dkt. Jafari ndiye mgombea aliyeteuliwa rasmi na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa 2025 Baada ya kuchukua fomu, amewashukuru viongozi na wanachama wa CCM kwa imani waliyoonyesha kwake na kuwaomba wananchi wa Jimbo la Busanda kumpokea kwa ushirikiano ili aweze kuwatumikia ipasavyo  “Nitakwenda kuisimamia vyema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kuhakikisha ndani ya Jimbo la Busanda inatekelezwa ili wananchi waendelee kufurahia maendeleo,” amesema Dkt. Jafari. Ameongeza kuwa ataimarisha mahusiano kati ya mwakilishi na wananchi na kuhakikisha Jimbo la Busanda linapendeza kwa miradi na huduma zitakazotekelezwa kup...

AMICI DELLA TANZANIA WATOA MSAADA WA KOMPUTA SHULE YA MSINGI KIPALAPALA

Image
  Na Allan Kitwe, DmNewsonline                  TABORA  TAASISI ya Amici Della Tanzania (Marafiki wa Tanzania) ya nchini Italia imetoa msaada wa komputa mpakato (laptops) 10 zenye thamani ya sh milioni 6 katika shule ya msingi Kipalapala iliyopo katika kata ya Itetemia Mjini Tabora. Akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule hiyo baada ya kukabidhi vifaa hivyo jana, Mwenyekiti wa Taasisi hiyo kutoka nchini Italia Hapiphana Lubangula amesema kuwa wametoa msaada huo ili kuboresha utoaji elimu katika shule hiyo. Amebainisha kuwa vifaa hivyo vitasaidia watoto wa shule hiyo kusoma kwa bidii na watakapomaliza shule ya msingi na kuendelea sekondari wawe na uwezo mkubwa wa kutumia komputa (tarakirishi).    Mbali na vifaa hivyo Lubangula amesema kuwa pia wanagharamia upakaji rangi kwenye vyumba vya madarasa vyote, ofisi za walimu na wataleta umeme katika shule hiyo ili kuwezesha watoto kusoma katika mazingira bora zaidi. Amesisiti...

COASTER KIBONDE AKIDHI VIGEZO,CHAMA CHA MAKINI CHAWASHUKURU WANANCHI

Image
   Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline            DAR ES SALAAM  CHAMA cha Makini kinapenda kutoa shukrani za dhati kwa wananchi wote waliojitokeza kwa wingi katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani kwa ajili ya kumdhamini Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama chetu. Zoezi la upatikanaji wa wadhamini lilianza rasmu tarehe 11 Agosti 2025,.mara baada ya Mheshimiwa Coaster Kibonde,Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Makini kuchukua fomu ya uteuzi.Zoezi hili limehitimishwa rasmi,tarehe 20 Agosti 2025 katika Mkoa wa  Morogoro na  kufuatiwa na kiapo Cha Mgombea huyo katika Mahakama Kuu ya Tanzania,hatua muhimu inayomwezesha sasa kukidhi vigezo vya kuendelea na mchakato wa uteuzi. Mgombea wetu anatarajia kurudisha fomu ya uteuzi rasmi tarehe 27 Agosti 2025  saa 3:30 asubuhi ,Jijini Dodoma na Kisha kusubiri uamuzi na uteuzi rasmi kutoka Tume Huru ya Uchaguzi. Tunatambua kwa dhati na kuthamini moyo wa uzalend...

Alhamdulillah ala kulli hal. Nimepokea uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa moyo wa shukrani. Quran Tukufu inatufundisha kuwa Allah ndie mpangaji na alipangalo ni bora kwetu. ALHAMDULILLAH. ----

Image
Ndugu zangu wanaTanga Mjini,              Na Mwandishi wetu, NITUMIE  fursa hii kuwashukuru kwa kuniamini kuwa Mbunge wenu kwa kipindi cha miaka 5 (2020 - 2025). Nafurahi kuona kuwa utumishi wangu kwenu umewagusa wengi na umeacha alama kubwa za kimaendeleo katika Jimbo letu. Asanteni kwa ushirikiano mzuri mlionipatia ktk kipindi chote cha Utumishi wangu. Kwa dhati ya moyo wangu, ninawashukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum wa CCM  Wilaya ya Tanga kwa kunipa kura nyingi ktk mchakato wa kura za maoni za kutafuta mgombea ubunge wa CCM katika Jimbo letu Tanga Mjini kwa kipindi cha 2025 - 2030. Mlinikopesha imani kubwa sana. Nitaienzi na kuithamini imani hii daima.  UAMUZI wa vikao vya Chama ni lazima UHESHIMIWE. Nampongeza Ndugu Kassim Amar Mbaraka (Makubel) kwa kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM Tanga Mjini. Ninawaomba wanakimji wenzangu hususani wanaCCM tumpokee na tumpe ushirikiano ili kuhakikisha ushindi wa kishindo kwa Rais Dkt Samia,...

OJAMBI MASABURI,KUPEPERUSHA BENDERA YA CCM JIMBO LA KIVULE ,KAMATI KUU CCM YAPITISHA JINA LAKE

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsonline             DAR ES SALAAM  CHAMA  Cha Mapinduzi (CCM)kimempitisha mwanachama  wa ambaye pia aliwahi kuwa Naibu instahiki Meya wa  Halmashauri ya Manispaa ya ilala Ojambi Didas Masaburi kuwa  Mgombea ubunge wa Jimbo la Kivule  jijini Dar es Salaam katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu. Masaburi ambaye aliongoza katika mchakato wa kura za maoni ndani ya Chama hicho ametangazwa kuwa mgombea ubunge katika Jimbo hilo  baada ya Kamati Kuu ya CCM kukaa kikao chake jijini Dodoma na kuchuja majina ya wagombea ubunge wake ambao watapeperusha bendera katika Uchaguzi huo. Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) CPA Amoss Makalla ametangaza majina ya wagombea ubunge katika majimbo yote ambapo katika  jimbo la Kivule Mgombea ubunge aliyepitishwa na Chama hicho    ni Ojambi Masaburi . Baada ya kupitishwa kwa jina lake Masaburi atachukua fom...