Posts

SERIKALI YAKEMEA VITENDO VYA UTEKAJI NA UNYANYASAJI KWA WATOTO

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhandisi Hamad Masauni amesema serikali haikubaliani na vitendo vyote vya utekaji na unyanyasaji wanavyofanyiwa baadhi ya watoto kwani  vitendo hivyo viovu vinaenda kinyume na utamaduni wa Taifa lenye utu, ustaarabu, amani na utulivu. Hayo yamebainishwa leo Julai 28,2024 Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Masauni wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu matukio ya vitendo vya ukatili na utekaji wa watoto amesema serikali imechukua hatua stahiki kwa wale wote waliobainika na itaendelea kuwachukulia hatua wale watakaobainika. “Hatua Kali zitachukiliwa Kwa wale wote watakaobainika kuhusika na matukio haya ya  kihalifu na tunaungana na Rais Dkt. Samia  Suluhu Hasan na watanzania wote wakiwemo wazazi na walezi kukemia vikali matukio haya ya kihalifu kwa watoto “ amesema Waziri Mhandisi Masauni. Aidha, ametoa rai kwa wananchi kushirikiana na Serikali husus...

KATIBU MKUU DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI MKAPA, CCM YATOA MILIONI 10 KUBORESHA MAJENGO YA SHULE LUPASO

Image
  Na Mwandishi Wetu,DmNewOnline MTWARA KARIBU  Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi ametembelea kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya 3, hayati Benjamin William Mkapa katika Kijiji cha Lupaso mkoani Mtwara, leo Julai 28, 2024, kuhani familia na kuzungumza na wananchi wa Lupaso. Balozi Nchimbi amesema “naomba nikiri kuwa mimi ni mwanafunzi wa hayati na nimekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Taifa (UVCCM), katika kipindi chake. Ndiye alinilipia ada ya kusoma chuo kikuu na alikuwa mfuatiliaji sana na alitulea vizuri. "Sio sisi tu, bali Watanzania wote aliwalea pia. Alikuwa mzalendo kwa nchi, alifanya mabadiliko makubwa kwa nchi yake na kwa Chama chake, lakini yote CCM chini ya Dkt Samia tutaendelea kuyaenzi yale yote aliyoyoacha hayati Benjamin Mkapa.  Pamoja na hayo nimeambiwa kero za hapa na tumezichukua. CCM inatoa shilingi milioni 10 kuanza kukarabati shule ya hapa Lupaso.” Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi n...

DAS SAME AWATAKA WANANCHI KUZINGATIA LISHE BORA,WASILE KUJAZA TUMBO

Image
Ashrack Miraji,DmNewsOnline SAME _KILIMANJARO    KATIBU  Tawala Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro,Upendo Wella amewataka wananchi kuzingatia ulaji wa vyakula vilivyoongezwa virutubishi lishe vitakavyosaidia kuboresha afya zao. Wella ameyasema hayo  wakati akimuakilisha Mgeni rasmi,Mkuu wa Wilaya ya Same,Kaslida Mgeni kwenye kikao cha matumizi ya vyakula vilivyoongezwa virutubishi kwa wadau wa lishe wilayani hapo. Amewataka wadau wa lishe kushirikiana kwa pamoja na watendaji kata na mdiwani kuitoa  elimu hiyo  kwa jamii inayowazunguka ili wajue  umuhimu na faida za kiafya kupitia kula vyakula vyenye virutubishi. "Jitihada ya serikali katika kupunguza matatizo ya lishe duni yanatokana na upungufu wa virutubishi muhimu ambayo ni madini ya chuma, madini ya joto na vitamin A. Hivyo niwaombe vongozi wote wa kata,viongozi madiwani ambao mmepata elimu hii,basi mkawahamasishe wananchi kwa maslahi mapana ya taifa letu" amesema. Katibu huyo amesisitiza kuwa ...

RAIS SAMIA KUONGOZA MKUTANO WA 15 WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM                    RAIS  wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuongoza Mkutano   wa 15 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) utakaofanyika Ikulu Jijini Dar es Salam kesho (Jumatatu). Akizungumzia mkutano huo muhimu wa baraza hilo jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mtendaji wa TNBC, Dkt. Godwill Wanga amesema mkutano huo unalenga kuangazia mazingira bora ya ufanyaji biashara na uwekezaji kupitia Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Mkumbi). “Kupitia mkutano huu, tunaenda kufanya tathimini ya mambo yote ambayo yamekuwa ni kikwazo katika kufanikisha  ufanyaji biashara na uwekezaji  nchini  sambamba na  kuja na mapendekezo ya nini kifanyike ili kuchochea matokeo chanya katika  kukuza na kuboresha   biashara nchini,”  amesema Dkt Wanga Aidha, Dkt Wanga amesema mkutano huu utapitia  ajenda za  mkutano wa 14 na kuangalia...

MNEC SALIM SAS KUIMARISHA CCM IRINGA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline IRINGA MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM (MNEC) Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas anatarajiwa kufanya ziara  maalum katika mkoa huo ambayo inalenga kuimarisha Chama na kukutana na Halmashauri Kuu za CCM Wilaya. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Iringa imebainisha kuwa ziara hiyo inatarajia kuanzia Mufindi siku ya Jumamosi tarehe 3, Agosti mwaka huu. "Agosti 3, 2024, Mufindi, Agosti 4  Kilolo, Agosti 7, Iringa Vijijini na mwisho atahitimisha Agosti 9, Iringa mjini," ilisema taarifa.  MNEC ASAS ameendelea kukiimarisha chama katika Mkoa wa Iringa huku akiwa nguzo kwenye kushiriki miradi ya kimaendeleo kimkoa, Nyanda za Juu Kusini pamoja na Taifa kwa ujumla. Pia ASAS anasifika kwa utendajikazi, upole, ustamilivu, subra, busara, huruma na mapenzi yake kwa chama na Taifa lake vimeendelea kumjengea taswira njema ya kwa wananchi wote. Aidha, amekuwa mstari wa mbele kwa kujitolea ka...

TMDA YAKANUSHA UWEPO PARACETAMOL INAYOBABUA NGOZI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline    MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imekanusha uwepo wa Dawa ya Paracetamol inayodaiwa kubabua ngozi. Kwa mujibu wa taarifa liyotolewa kwa umma na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, imesema taarifa iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uwepo wa dawa hiyo, haina ukweli na kuwataka wananchi waipuuzie. Akinukuu taarifa hiyo Dkt Fimbo amesema hadi sasa wao kama makala hawajatambua dawa hiyo na kuwataka wananchi kusambaza taarifa za uongo ambazo zinaleta taharuki. "Dawa hiyo inadaiwa kuwa ni paracetamol mpya nyeupe sana na inayong'aa, madaktari wanashauri kuwa ina virusi vya "Machupo", inayochukuliwa kuwa moja ya virusi hatari zaidi ulimwenguni na kiwango cha juu cha vifo. Aidha, mtoa taarifa anaitaka jamii kuisambaza taarifa hiyo kwa kila mtu aliyeko katika orodha yake ya mawasiliano ili kuokoa maisha. Anamalizia kwa kusema ‘’Nimefanya  sehemu yangu, sasa ni zamu yako. Kumbuka kwamba Mungu huwasaidia wale wanaosaidia we...

THE REDS YASAIDIA YATIMA MOROGORO

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline MOROGORO  KATIKA kusherehekea siku ya Klabu ya Simba Agosti 3,2024, Kundi  Sogozi la The Reds Community ambalo linahusisha wanachama na washabiki wa timu hiyo limetembelea na kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Kituo cha Watoto yatima cha Raya kilichopo Lugono mkoani  Morogoro. Msaada huo wa wana Simba umewasilishwa leo  Julai 27 ,2024 na Mwenyekiti wa  The Reds Community, Zahran Rashidi akiwa ameambatana na wana kundi kwa niaba ya kundi hilo ambalo limedhamiria kuonuana kiuchumi na kijamii. Mwenyekiti huyo amesema kundi la The Reds Community limeanzishwa na wana Simba kutoka pande zote za nchi na nje ya nchi kwa lengo la kusaidiana, hivyo katika kuelekea siku ya Simba wameamua kuchangishana fedha ambazo zimenunua mahitaji mbalimbali kwa ajili ya kusaidia watoto yatima 90 wa Kituo cha Raya. "Sisi The Reds Community tunaamini jamii ni muhimu na kwa kuthibitisha hilo tumeweza kuchanga takribani Shilingi miloni 1.5 ambazo zimetumika k...